The House of Favourite Newspapers

Wema: Wamekubali Wembamba Wangu

MKALI wa filamu za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’, amesema miezi kadhaa nyuma watu walikuwa wakimbeza kutokana na kukondeana, lakini sasa wameukubali wembamba wake.

Akichonga na Shusha Pumzi, Wema alisema, siku za nyuma alikuwa akikutana na maoni mengi kwenye ukurasa wake wa Instagram ambapo watu walikuwa wakimshauri kurudisha mwili wake wa zamani (unene), lakini sasa wanamwambia awaelekeze kitu alichotumia hadi akakonda kwani amependeza.

 

“Sasa hivi kila mtu anaukubali wembamba wangu na kuupenda hivyo nao wanaomba ushauri wawe kama mimi,” alisema Wema.

Stori: Imelda Mtema

Comments are closed.