×

Ally Rehmtullah Aja na Gia Mpya Ya Vazi la Kitenge

Ally Rehmtullah akizungumza wakati wa hafla hiyo.

Mbunifu maarufu wa mitindo hapa nchini Ally Rehmtullah, jana alikuja na gia mpya kwa kufanya hafla ya kuwaunganisha wabunifu wa vazi la kitenge na kufanya nao kazi pamoja.

Sehemu ya nguo zikiwa dukani hapo.

Akizungumza na mwandishi wetu, Ally Rehmtullah amesema anawakaribisha wabunifu hao kufanyakazi zao kwenye duka lake lililopo Mtaa wa Chole, Masaki Dar na kuuzia kazi zao kwenye duka lake bila gharama yeyote.

Amesema lengo la kuwaunganisha wabunifu hao ni kuwajengea uwezo na kubadilishana ujuzi ili kuendeleza fani hiyo.

Mafundi wake wakiwa kazini.
Rehmtullah akibadilishana mawazo na mmoja wa wageni waalikwa.
Hafla ikiendelea.
Wabunifu wa mitindo maarufu nchini, Hadija Mwanamboka (kushoto) na Mustafa Asanali wakibadilishana mawazo na Rehmtullah kwenye hafla hiyo.
Mwanamitindo wa kimataifa, Flaviana Matata naye akiwasili eneo la tukio.

HABARI: Neema Adrian PICHA: Richard Bukos/GPL

Leave a Comment