×

Mgonjwa wa Corona Atoroka Hospitali, Mtandao Wake Wasakwa

SERIKALI ya  Kenya inawasaka watu 85 wanaohofiwa kuambukizwa virusi vya Corona baada ya kuambatana na mgonjwa wa virusi hivyo katika hospitali ya Mbagathi.

 

Mgonjwa huyo anasemekana kutoroka katika wodi iliyotengwa kwa ajili ya wagonjwa wa Corona katika hospitali hiyo ila alikamatwa baadaye na maafisa wa ulinzi.

Katibu mkuu wa muungano wa wauguzi nchini humo, Seth Panyako, alithibitisha kisa hicho kupitia  hotuba yake na wanahabari jana Jumatano, Machi 18.

 

“Kuna mgonjwa aliyepelekwa katika hospitali ya Mbagathi akiwa na virusi hivyo, aliondoka hospitalini humo bila kupewa ruhusa lakini maafisa wa ulinzi walifanikiwa kumkamata. Kwa sasa tunawasaka wagonjwa wengine 85 waliotangamana naye,” Panyako alisema.

Leave a Comment