×

Bonucci Amkingia Kifua Ronaldo

BEKI wa Juventus, Leonardo Bonucci, amesema hawaelewi watu wanaomshangaa Cristiano Ronaldo kukosa penalti kwani ni kitu cha kawaida.

 

Juzi Ijumaa, Juventus ilicheza mchezo wa Coppa Italia dhidi ya AC Milan na Ronaldo alikosa penalti kwenye mechi hiyo iliyomalizika kwa suluhu, lakini Juventus imetinga fainali baada ya mechi ya kwanza kuisha kwa 1-1.

 

“Hata wachezaji wakubwa huwa wanakosa penalti kwa hiyo mimi sioni kama ni ajabu.

“Cristiano kwetu ni mchezaji muhimu sana na kwanza alikuwa anawapa presha kubwa wapinzani wetu.

 

“Sema hatukuwa na bahati tu kwa sababu kipa wa AC Milan, (Gianluigi) Donnarumma alifanya vizuri. Tulipambana, lakini Milan wanastahili pongeza licha ya kucheza pungufu,” alisema Bonucci.

TURIN, Italia

Leave a Comment