MWONGOZAJI maarufu wa video Bongo, Director Hanscana, hupenda kuongea na mashabiki zake kupitia instagram na kuruhusu mashabiki kumuuliza maswali.
Jana Jumatano, Novemba 11, 2020, alitoa nafasi hiyo ambapo shabiki mmoja alimuuliza: “Bado Unasimamia Waimbaji Katika Ile Lebo ya Hanscana Brand?”
Majibu ya Hanscana yalikuwa: “Hapana na sirudii, nimekoma.”
Marioo ni mmoja wa wasanii waliokuwa wanasimamiwa na Hanscana Brand ila kwa sasa hawafanyi kazi pamoja. Si Hanscana wala Marioo ambaye ameeleza kwa nini waliacha kufanya kazi pamoja. Kufahamu zaidi hayo pamoja na mengine mengi, kaa karibu na Global TV Online
