×

Watumishi 90,000 Kupandishwa Madaraja

Serikali inatarajia kupandisha madaraja watumishi wa Umma 90,000 nchi nzima lengo likiwa ni kutimiza takwa la kisheria linalotaka watumishi waliokidhi vigezo kupandishwa madaraja.

 

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora, Deo Ndejembi wakati akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino.

 

Licha ya kutoa ahadi hiyo, pia amewataka Watumishi kufanya kazi kwa weledi wakifuata taratibu, miongozo na maadili ya umma, huku akisisitiza kuwa Serikali haitomvumilia Mtumishi yeyote atakayekiuka miiko na sheria za kazi.

 

Leave a Comment