The House of Favourite Newspapers

Bocco Awafunika Kagere, Chris Mugalu Simba

0

NAHODHA wa Simba, mzawa John Bocco ameandika rekodi yake ya kufunga mabao mengi kwa muda mfupi aliotumia ndani ya uwanja tofauti na washambuliaji wengine ndani ya kikosi hicho.

 

Akiwa amecheza jumla ya mechi 23 kwenye ligi pamoja na Ligi ya Mabingwa Afrika ametupia jumla ya mabao 14 jambo linaloonyesha kwamba ana ushkaji mkubwa wa kucheka na nyavu pale anapopata nafasi ya kucheza.

Meddie Kagere, nyota wa Simba ambaye anapambana kutetea kiatu cha ufungaji bora alichotwaa msimu uliopita yeye ametupia jumla ya mabao 14 kwenye mechi 31 ambazo amecheza.

 

Msimu uliopita alitupia jumla ya mabao 22 katika ligi na kutwaa kiatu cha ufungaji bora ila msimu huu ametupia mabao 11 na kinara wa utupiaji ni Prince Dube wa Azam FC mwenye mabao 14.

 

Chris Mugalu, yeye ndani ya Simba amefunga jumla ya mabao 11 akiwa amecheza mechi 22 kwa msimu wa 2020/21, hivyo rekodi zinaonyesha kwamba kwa washambuliaji wote watatu, Bocco amewafunika wote kwa kuwa amecheza mechi chache ila amefunga mabao mengi katika muda alioupata chini ya Kocha Mkuu, Didier Gomes

Leave A Reply