
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, Ashiriki Katika Kongamano la Kumbukizi ya Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Rais Benjamin William Mkapa.
“Hayati Mzee Mkapa alitoa fursa zaidi kwa Sekta Binafsi na kukaribisha uwekezaji kutoka nje. Hatua hizi zilisaidia kuongeza mapato ya Serikali kutoka TSH Bilioni 331.2 kwa mwaka 1995 hadi kufikia TSH Trilioni 2 kwa mwaka 2005”
“Mzee Mkapa alifanikiwa kupunguza Deni la Taifa kutoka 143.7 % ya pato la Taifa tulilokuwa tukidaiwa mwaka 1995 hadi 60.7% mwaka 2005 na hii ni baada ya Mzee Mkapa kuzishawishi Nchi Wahisani na Taasisi za Kifedha za Kimataifa kutusamehe madeni”
“Hii iliwezekana baada ya kutumia uwezo wake wa diplomasia kuzishawishi taasisi za kifedha za kimataifa na nchi wahisani kusamehe madeni kutumia mpango wa HIPC (Heavily Indebted Poor Countries) uliosimamiwa na Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la IMF”
“Mzee Mkapa alifanikiwa kupunguza deni la taifa kutoka 143.7% tuliyokuwa tukidaiwa mwaka 1995 hadi 60.7% mwaka 2005”
⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP: ⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8 ⚫️ iOS:https://apple.co/38HjiCx