
UONGOZI wa Klabu ya Yanga umepanga kuzindua Wiki ya Mwananchi Agosti 22 visiwani Zanzibar ambapo kilele chake kitakuwa Agosti 29, jijini Dar es Salaam.
Ofisa Habari na mawasilano wa Yanga, Hassan Bumbuli amesema kuwa malengo makubwa ni kushirikiana na mashabiki na wapenzi wa timu hiyo huku wakitoa misaada mbalimbali kwa jamii yenye uhitaji maalumu.
