




Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Amos Makalla leo amepokea mbio maalum za Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa Ndege wa Mwl JK Nyerere Terminal 1 ukitokea Mkoa wa Pwani.
Akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mhe Abubakar Kunenge Mkuu wa Pwani , Mhe Amos Makalla amesema Mwenge wa Uhuru utakimbizwa umbali wa KM 355.6 ukizindua na kuweka jiwe la msingi katika miradi ya Maendeleo ipatayo 46 iliyokamilika na iliyoko katika hatua za utekelezaji yenye thamani zaidi ya Bilioni 105.
Baada ya kukimbizwa katika Wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam, Agosti 23, 2021 Mwenge wa Uhuru utakabidhiwa katika Mkoa wa Lindi.
Aidha Mhe Mkuu wa Mkoa amekabidhi Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Ilala tayari kwa kuanza kukimbizwa ndani ya Wilaya za Mkoa wa Dar es Salaam.
Imetolewa na: Kitengo cha Habari na Uhusiano Ofisi ya Mkoa wa Dar es Salaam