The House of Favourite Newspapers

Kenyatta Kuwa Rais wa Kwanza wa Afrika Kukutana na Biden

0

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta atakutana na rais wa Marekani Joe Biden wakati akimaliza ziara yake ya siku mbili nchini Marekani.

 

Rais Kenyatta atakuwa rais wa kwanza kutoka Afrika kukutana na rais Biden tangu kiongozi huyo aapishwe mwaka huu.

 

Msemaji wa Ikulu ya Kenya amesema viongozi hao wawili watajadili mambo mbalimbali yakiwemo masuala ya amani , usalama na mabadiliko ya tabia nchi.

 

Jumanne, Rais Kenyatta aliwaongoza viongozi wa biashara kusaini mikataba kadhaa ya uwekezaji wa biashara ndogo na wastani pamoja na miradi ya usafirishaji na nishati safi.

 

Marekani inaiona Kenya kuwa mshirika sahihi katika kupambana dhidi ya ugaidi katika eneo la Mashariki mwa Afrika.

 

View this post on Instagram

 

A post shared by Global Publishers (@globalpublishers)

Leave A Reply