×

Mawakili wa Mbowe Wambana Shahidi wa Serikali

Fredy Kapala shahidi wa tano wa upande wa Jamhuri katika kesi ya tuhumza za ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu ametoa ushahidi katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi.

 

Kapala aliyejitambulisha kuwa ni mwanasheria wa Kampuni ya Mawasiliano ya Tigo ametoa ushahidi huo leo Jumanne Novemba2, 2021.

 

Ifuatayo ni sehemu ya ushahidi:

 

Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Kabla hatuja Anza Maswali ya Dodoso nilikuwa naomba Mahakama itambue Uwepo wa Wakili Mwenzangu Nashon Nkungu.

 

Jaji anaandika Kidogo..

Mtobesya: nilikuwa naongea na wenzangu kama Tutapata mapumziko ya Afya lakini naomba Niulize mimi Japo kwa nusu saa tu baada ya Hapa Nina kesi mahakama ya Rufani nitaacha wenzangu waendelee

Jaji: itakuwa vizuri ukituma Dakika 20

Mtobesya: Shahidi Wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali ulielezea kwa urefu sana Namna ambavyo Mnafanya kulinda Mfumo wenu Pamoja na Server, Je Ni sahihi

 

Shahidi: Ni sahihi

Mtobesya: Lakini Hukuiambia Mahakama Mpaka Wakati Unatoa Taarifa hapakuwa pamefanyika Audit ya namna gani na Kwamba System Ilikuwa Vizuri

Shahidi: Sahihi

Mtobesya: sikusikia Ulisema Kwamba Servers zinaweza kuingiliwa na Mahakama

Shahidi (Tigo): Sahihi

 

Mtobesya: Wakati Jaji akiandika elezea HACKERS ni Watu gani

Shahidi (Tigo): ni Wataalamu wa Mitandao ambao wanasoma Mfumo au Wanakuwa wanamfahamu Mfumo na Wanatabia ya kujaribu Kuingia Kwenye Mfumo, Kuchukua ama Kuharibu Taarifa ama Mfumo Wenyewe

Mtobesya Nitakuwa sahihi nikisema wakati Unaongozwa na Wakili Wa Serikali Hukusema kama palikuwa na Possibility za Hackers Kuingia Kwenye Mfumo

 

Shahidi (Tigo): Ndiyo Sikusema

Mtobesya: Nitakuwa sahihi Nikisema Hackers Wanauwezo wa Kuingia na Kucheza na Taarifa za READ ONLY kama alivyokuwa anakuongoza Wakili wa Serikali

Shahidi (Tigo): Ndiyo Uwezekano Upo

Mtobesya: Ofisi ya Tigo ulisema ni nini

 

Shahidi (Tigo): Jina la Kibiashara

Mtobesya: Ofisini kwenu kuna wanasheria Wangapi

Shahidi (Tigo): Kwa Ujumla au Legal Department.?

Mtobesya: Legal Department

Shahidi (Tigo): Watatu

 

Mtobesya: Nilisikia Ulisema wanaweza Kuingia Kwenye Mfumo ni watu wa Mantainance na Audit, Je Kuna lolote Umetoa lenye Jina lako kwamba wewe ndiyo ulishughulikia Taarifa hizi

Shahidi (Tigo): Mbali na Barua kwa kweli Hakuna

Mtobesya: na Barua pia haina Jina

Shahidi (Tigo): Ndiyo haina Jina

 

Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Barua ithibitishe hiyo

Mtobesya: Nitakuwa sahihi Nikisema Kwenye Taarifa ya KYC (KNOW YOUR CLIENT) haihitaji Barua za Utambulisho kama Serikali za Mitaa

Shahidi (Tigo): Hapana haihitaji

Mtobesya: tuweke Record sawa kwa hiyo hata Photocopy Ya Kitambulisho Cha NIDA haihitajiki

Shahidi: NI Scanned ID

 

Mtobesya: Nitakuwa Sahihi nikisema KYC inatakiwa iambatane na hiyo Image ya Kitambulisho Cha NIDA

Shahidi (Tigo): Siyo lazima

Mtobesya: Nitakuwa sasa Kwenye Kielelezo namba 09 Cha Mtu Uliye Sema ni Freeman Mbowe Taarifa zake Hazipo

Mheshimiwa Jaji naomba Kielelezo namba 09

Mtobesya: Nionyeshe Jina la Mtumishi aliyesajili

 

Shahidi (Tigo): Siyo Mtumishi ni Mtu Mwenye Device

Mtobesya: Ndiyo huyo huyo Nionyeshe Jina lake

Shahidi (Tigo): Halipo

Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema hata Mtu aliye sajili haionekani alisajilia wapi?

Shahidi (Tigo): Ndiyo

 

Mtobesya: Kwa Niaba ya Mshitakiwa wa kwanza Naomba Kumaliza

Mallya: Shahidi wewe ni Wakili siyo

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Mallya: Umekuwa Admitted Kwenye Bar Mwaka gani

Shahidi (Tigo): 2013

Mallya: Tigo Umeajiliwa lini

 

Shahidi (Tigo): 2012

Mallya: na Uliajiriwa Department gani

Shahidi (Tigo): Legal Department

Mallya: Ulitaja Department Zingine Kwenye Ushahidi wako

Shahidi (Tigo): Ndiyo Kama IT Security

Mallya Kazi zake..?

 

Shahidi (Tigo): Ulinzi wa Taarifa za Mfumo na Taarifa zote zinazoshughulika na wateja

Mallya: hiyo Department ya Security Bwana Yahaya Zahoro ndiye anayeshughulikia Taarifa kama hizi

Shahidi (Tigo): Yeye ni Internal Investgation Officer

Mallya: yeye ndiye anaye Shughulikia Maswala kama haya

Shahidi (Tigo): Siyo haya

 

Mallya: kuna Department inayoshughulika na Masuala External Investigation

Shahidi (Tigo): hatuna, hiyo labda ni Polisi na Serikali

Mallya: Ulizungumza lolote kuhusu Telepin

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Mallya: Ulisema ni nini

 

Shahidi (Tigo): Mfumo Mmoja Ulikuja Kure place Mwingine

Mallya: Upi Ulianza

Shahidi (Tigo): Ulianza CONVIVER Ukaja Telepin

Mallya: kwanini waliondoa CONVIVER

 

Shahidi (Tigo): Kwa sababu ya Mabadiliko ya muda na Technology

Mallya: Wakati Unatoa Exhibit P8 suala la Miamala ya Fedha Ulielezea Mahakama Kwamba Ulizungumza Kutoka Kwenye Software gani

Shahidi: Screen Server

 

Mallya: wakati Unaona hizi Taarifa Ulisema Umetumia Mechanism Gani Kugenerate hii Print Out

Shahidi: Nilichagua Option ya Kuprint

Mallya: Kwanini Ulichagua Kwanini Uliacha Option Ya Screenshort ukaamua Kuprint

Shahidi (Tigo) Ilikuwa ishu ya Choice tu

 

Mallya: Kuhusiana na Jina lako Mwanzoni palikuwa na Maombi ya Kubadili Kutoka Frank Kwenda FREDY,

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Mallya: Je Kapala ni R au L Mwishoni

Shahidi (Tigo): NI L Mwisho

Mallya: Kwa hiyo huyu Kapara siyo wewe

 

Shahidi (Tigo): Inaweza Kuwa wamechanganya

Mallya: Wewe ni Wakili unajua Madhara ya kukosewa Jina

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Mallya: Life cycle ya Simu Card unaweza Kupata Wapi

Shahidi (Tigo): SQL server

 

Mallya: Mimi ninao Ushahidi inapatikana Kwenye SMAP

Shahidi (Tigo): Ndiyo inapatikana pia

Mallya: Unababilisha Jibu eeh!

Shahidi (Tigo): Hapana Kote unaweza Kupata Kote

Mallya: Taarifa uliyoileta KYC ni Taarifa Accuracy?

Shahidi: Ndiyo

 

Mallya: Unataka Mahakama Ikueleweje ukisema Accuracy

Shahidi: Nimezipata Kwa Njia iliyokamilika sina Wasiwasi nazo

Mallya: Hapo Kuna Mpangilio wa Taarifa Je umeelezea Sababu Ya Kupanga hivi

Shahidi: Hapana

 

Mallya: Kuna City imeandikwa Kilimanjaro Je Ulimwambia Jaji hiyo Kilimanjaro City Unaifahamu

Shahidi (Tigo): Hapana

Mallya: hiyo Kilimanjaro City unaifahamu

Shahidi (Tigo): Hakuna Kilimanjaro City

Mallya: Kuna District inaitwa Kinondoni, Je huko Kilimanjaro inaweza kuwa District ya Kinondoni?

Shahidi (Tigo): SAMAHANI KIDOGO

 

Mallya: NISHAKUSAMEHE

Shahidi (Tigo): RUDIA SWALI

Mallya: Kuna City ya Kilimanjaro, kuna District ya Kinondoni

Shahidi (Tigo): hakuna

Mallya: Kuna sehemu hapo imeandikwa Region, Region gani?

 

Shahidi ( @Tigo_TZ ): Kimyaaaaaaaaaa

Mallya: Je huko Dodoma Kuna Sehemu Inaitwa Kilimanjaro City?

Shahidi (Tigo): Hakuna

Mallya: Unasemaje Kuhusu hizo Taarifa

 

Shahidi (Tigo): Kuna Taarifa ambazo zipo NIDA so Ukiweka Kidogo Nauliza Mfumo wa NIDA, Mtu Mwenye Jina hili na Fingerprints hizi Zina Match

Zinasoma anaitwa nani, na Taarifa zake zote zinakuja Kama hazipo zinakuja Kuhuishwa siyo Za NIDA Kama hazipo ni za kwetu sisi

Mallya: kama Taarifa hakuna Je Freeman Mbowe alijisajili Mwenyewe

Shahidi: Nahisi Wakili hatuelewani katika hili, Nilisha Sema Kama Taarifa zilizotakiwa Kuchukuliwa NIDA kama Hawana Sisi tulipaswa kuchukua NIDA

 

Mallya: Kielelezo 09 kimetoka kwenu au NIDA

Shahidi: kwetu

Mallya: Kwa hiyo Hiyo Mitambo ya kuprint ipo NIDA au Ofisini Kwenu

Shahidi (Tigo): Ofisini Kwetu

Mallya: Aliyemsajili Mbowe nani kama Kweli Mbowe ana namba ya Tigo

Shahidi (Tigo): Simjui

 

Mallya: Kwanini humjui

Shahidi (Tigo): Sababu Kwenye Taarifa hiyo Sijamuona

Mallya: Nitakuwa sahihi Nikisema Taarifa Yenu Haipo Kamili nitakuwa Sahihi

Shahidi (Tigo): Haupo Sahihi

Mallya: pale Ofisini Kuna Department ya Tigo Pesa

Shahidi (Tigo): Ndiyo

 

Mallya: Ulizungumzia kuhusu Tigo Pesa Department.?

Shahidi (Tigo): Siku zungumzia

Martin Maranja Masese @IAMartin_ · 2h Mallya: Mimi siiijui kama namba ni ya Freeman Mbowe au Lah, lakini hebu niambie Pale Kwenu Kuna Kitengo cha Business to Business kama Post paid

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Mallya: Ulizungumzia Hiyo

 

Shahidi (Tigo): Hapana

Mallya: Hii namna ya Kujibu Mabarua ni Standard Form au Kila Barua na namna yake

Shahidi (Tigo): NI Standard Form

Mallya: Lengo la Kuweka ENEO la Kujaza Kosa la Mteja wenu wanalomchunguza nalo

Shahidi (Tigo): NI Format ya Kuweka Kosa wanalo mchunguza nalo

 

Mallya: Je Polisi Wakitaka Uwape Taarifa ya kuchunguza Girl Friend wake we utatoa taarifa

Shahidi (Tigo): Hapana

Mallya Je wewe Ulipata Kuuliza Wana mtuhumu Kwa Makosa gani

Shahidi (Tigo): Hapana Sikuuliza

Mallya: Kwa hiyo wewe Ukatoa Taarifa hata akama Mtu anataka Kujua namtumia pesa Mpenzi wake

Shahidi (Tigo): Siyo Utaratibu wangu wa Kazi

 

Mallya: Kwa hiyo nyie Tigo manataka Kutuambia Kuwa Polisi Wakitaka Taarifa hata kama hawana Kosa la Kuchunguza Mtawapa

Shahidi (Tigo): Siyo lazima pawe na kosa la Jinai, Kazi yangu ni kuona Kama Wamekidhi vigezo

Mallya: Ni Mara yako ya Kwanza Kupata Barua Kutoka Forensic Bureau

Shahidi (Tigo): Hapana

Mallya: Kwani Forensic Bureau Wanahusika na masuala ya ndoa na matunzo ya watoto?

Shahidi (Tigo): Mimi naangalia namba na kutoa taarifa

Mallya: Hukuona umuhimu wa kujua kosa..?

 

Shahidi ( @Tigo_TZ ): Siyo kazi yangu kujua makosa

Mallya: Mheshimiwa Jaji ni hayo tu

Jaji; anaandika Kidogo

Jaji; Tutaenda break Dakika Ngapi

Kibatala: Ngoja tushauriane

Jaji; Sawa

 

Wakili wa Serikali; Tumekubaliana na Wenzetu Tubreak Kwa Dakika 40 turudi saa 08 kamili

Jaji; basi tunabreaka kwa Dakika 40 tutarudi Saa 08 kamili, Naomba tutunze Muda

Mallya: Je KAPALA ni R au L Mwishoni?

Shahidi: NI L Mwisho

Mallya: Kwa hiyo huyu KAPARA siyo wewe?

Shahidi: Inaweza Kuwa wamechanganya

Mallya: Wewe ni Wakili unajua madhara ya kukosewa Jina?

 

Shahidi: Ndiyo

Jaji ameingia tena

Kesi inatajwa tena.

Kibatala: Naomba Wakili Dickson Matata Kwa Ruhusa yako aingizwe Katika column

Nilimuombea Ruhusa Kwamba atachelelewa na Kwa Sasa ameshafika

 

Namualika Wakili wa Mshtakiwa wa 03 aweze Kuuliza Maswali ya Dodoso

Matata: Nilikusikia Kwamba Kwenye Kitengo Cha Sheria Mpo watatu

Matata: Wakati Unahojiwa na Wakili wa Serikali Ukusema nani Mkuu wa Idara Yenu

Matata: Na Hukusema Wewe licha ya Kuwa Mwanasheria Ni Mkuu wa Idara, Kweli siyo kweli

Shahidi (Tigo) +/ Siyo Kweli

 

Matata: licha ya Kuwa Wewe Mwanasheria Hukusema Wewe unanafasi gani Nyingine

Shahidi: Siyo Kweli

Matata Ikae hivyo hivyo Mheshimiwa Jaji

 

Matata: wewe Ndiyo umepokea Barua, wewe Ndiyo umeprint Taarifa, na Wewe Ndiyo Umepeleka Majibu Polisi

Shahidi (Tigo): Sijaelewa

Matata: Wewe Ndiyo ulipokea Barua

Shahidi (Tigo): Sahihi

Matata: wewe Ndiyo uliandika Barua

Shahidi (Tigo): Ndiyo

 

Matata: Nitakuwa sahihi nikisema wewe Ulifanya Kila Kitu Kwa Niaba ya Tigo

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Matata: Ulielezea Mahakama Kwamba Kwanini Wenzio 3 hawakushiriki katika hiyo kazi

Shahidi (Tigo): Siyo kweli

 

Matata: kampuni yenu mnasera ya Usiri?

Shahidi (Tigo): Upo sahihi

Matata: ambapo Mawasiliano ya mteja yanakuja ni Siri kati ya Mteja na Nyinyi

Shahidi (Tigo): Sahihi

Matata: Kwamba nitakusa sahihi nikisema Moja ya Sababu Ya Kuvunja Usiri ni endapo panahitajika Kufanya Uchunguzi Kwa VYOMBO Vya Uchunguzi

Shahidi (Tigo) Sahihi

 

Matata: Na Utoaji huo Wa Taarifa unalindwa na Sheria

Matata: Na wewe ni Mwanasheria

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Matata: Na Mimi nimekusikia Mtatoa Taarifa Endapo Mtaombwa au Kwa Amri ya mahakama

Shahidi (Tigo): Sahihi

 

Matata: Kwa kuzingatia Umuhimu wa Usiri wa mteja Nisomee Kifungu cha 34 cha Sheria Ya a Makosa ya Mtandao

Shahidi (Tigo): 34(i) Disclosure of Data………

Matata: Utakubaliana na Mimi kwamba Pale panapohitajika Taarifa Ya Uchunguzi Police ambaye ni Ofisa anaweza Kuomba Taarifa Kwenu

 

Shahidi (Tigo): Hapo anaongelea Ongoing Trafficking Data siyo Stored Data

Matata: Mh Jaji naomba Kielelezo

Matata: hiyo Barua Wametumia Kifungu gani

Shahidi (Tigo): Kifungu cha 34 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao

Matata: Na Mimi nimekuuliza Usome Kifungu gani

 

Shahidi (Tigo): Kifungu hicho hicho cha 34

Matata: Kwa hiyo utakubaliana na Mimi wewe Umeombwa Kitu Kingine na wewe Ukatoa Kitu Kingine

Matata: Kwa Mujibu wa Maelezo yako walitaka Uwapo Data Trafficking Ya Siku hiyo Siyo Stored Data

Matata: naomba Unisomee hapa

Shahidi kutoka @Tigo_TZ anasoma kwa sauti sheria tajwa

 

Matata: Utakubaliana na Mimi kwamba Kama Mtu ameombwa Taarifa na akakataa na Yule Police Officer alitakiwa kwenda Mahakamani Kuomba Court Order

Shahidi (Tigo): NI sahihi

Matata: Naomba Unionyeshe Kwenye hii Barua ni wapi Pameonyeshwa Kosa Kwenye hiyo Barua ambapo hiyo namba Inatuhumiwa kwenye Kosa la Jinai

Shahidi: Hakuna

 

Matata: Kuna Kosa Umeandika hapa Wakati Unajibu Barua hii Kuhusiana na Uchunguzi

Shahidi (Tigo): Kuna Dash Hakuna Kosa

Matata: Kwa hiyo Hakuna Kosa

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Matata: Pamoja na Barua kuja Bila Kutaja Kosa na Wewe Ukatoa Taarifa hiyo bila Kutaja Kosa kama Inavyosema katika Kifungu 34

 

Je Hukuona hilo ni Jambo lisilostahili ili uwakatalie Waende Mahakamani Kulinda Usiri wa wateja wenu

Shahidi (Tigo): Hapakuwa na Haja hiyo

Matata: Kwa hiyo Polisi Wakikuandikia Barua ya Kutaka Taarifa Bila Kukutajia Makosa

Shahidi (Tigo): Nitampa

 

Matata: Kwenye kampuni yenu haitaji la Kutuma Meseji au Kupiga Simu Kwenu ni Kosa

Shahidi (Tigo): Hapana Siyo Kosa

Jaji: wakili wa mshtakiwa namba 4

Kibatala: Nyie Kama @Tigo_TZ MIC Tanzania Ltd Priority ni nini, USIRI wa MTEJA au Kufuata MASHARTI ya POLISI?

Shahidi (Tigo): Tuseme COMPLIANCE na SIRI za MTEJA

Kibatala: Sawa tuweke hivyo Kwenu Kipaumbele ni nini?

 

Shahidi (Tigo): COMPLIANCE

Kibatala Unafahamu Kuwa Mtu uliyemtolea Ushahidi Kama Freeman Mbowe Kuwa ni Kiongozi wa Chadema kama Kiongozi wa Chama Cha Upinzani

Shahidi (Tigo): Simfahamu

Kibatala: Umekuwa Wakili tangu lini

Shahidi (Tigo): 2013

 

Kibatala: Bado unataka tukubali kuwa humfahamu Freeman Mbowe kama Kiongozi wa Chadema, chama kikuu cha upinzani Tanzania?

Shahidi (Tigo): Ndiyo sifahamu, Wapo wengi

Kibatala: Barua ilisema Kwamba iwe ni Siri sana Mteja asijue?

Shahidi (Tigo): Haiku Sema hivyo

 

Kibatala: Ulimtaarifu Mteja Mwenyewe kwamba Kuna Taarifa zako za Kiuchunguzi zinahitajika

Shahidi: Hapana

Kibatala: Kama Kampuni Mlichukua Hatua yoyote ya Kumlinda Mteja Kwa kwenda Mahakamani Kupinga au Kuandika Barua kwenda TCRA, Mlichukua hatua kama hiyo

Shahidi: Hapana

 

Kibatala: mlichukua hatua gani kumlinda mteja

Shahidi (Tigo): Hiyo siyo kazi yetu, Hakuna hatua tuliyoichukua kumlinda mteja

Kibatala: Mnafahamu Angalau kuwa Kuna Tasisi Mbili angalau zinahusika Kulinda Maslahi ya Mteja

Shahidi (Tigo): Ndiyo nazifahamu

Kibatala: Zitaje

 

Shahidi (Tigo): TCRA na FCC

Kibatala: Hakuna Polisi Wana abuse power zao

Shahidi (Tigo): Sifahamu

Kibatala: Barua Yako uliyoitoa Mahakamani, Je Mahakama Ikitaka Kujua Kuwa nini wewe Mmiliki wa Barua, Ina angalia Wapi

 

Shahidi: Kielelezo namba p6

Kibatala: Msaidie Mheshimiwa Jaji akiangalia Wapi ataona Barua hii Umesaini wewe FREDY Kapala

Shahidi (Tigo): Barua Yenyewe Ilipotoka ni MIC Tanzania Ltd na Pia Nimesema ni Saini Yangu

Kibatala: Mimi nasema Hakuna Mahala Popote pale ambapo Pana Majina yako Katika Kielelezo namba p6

Shahidi (Tigo): Ndiyo Hakuna Majina

 

Kibatala: Je Uliongozwa na Wakili wa Serikali Kutoa Nyaraka Nyingine Kufanya Ulinganifu kwamba hii ni Saini yako

Shahidi (Tigo): Sikuyatoa

Kibatala: Unakubaliana na Mimi Kuwa Hatuna sehemu ya Kulinganisha Signature Yako

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Kibatala: Tuchukulie Kwamba Barua Iliandikwa na Polisi na wewe hii ni Saini Yako, Je ni wapi Mheshimiwa Jaji akiangalia anaweza Kuona Barua hii Ilipita kwa Wengine Tigo kwamba Ufanye kama kwa Ku’ minute

Shahidi (Tigo): Sijaelewa

 

Kibatala: Unafahamu Kuwa baadhi ya Ofisi Barua inatembea na kupelekwa kwa Mhusika baada ya Kupita kwa wengine

Ulimwambia Jaji kama Nyie Tigo hamna Utaratibu huu

Shahidi: Siku Mwambia

Kibatala: Unakubaliana Barua Yako ya Tarehe 02 Haielei hewani Ndiyo Maana Inaviambatanishi

Shahidi (Tigo) Ningeweza Kujibu Lolote

 

Kibatala: Taja Kwa Nguvu hiyo kumbukumbu namba ya katika Barua ya Polisi Kama kiambatanisho p6

Kibatala: Msomee Jaji Sasa Nyaraka ambayo wewe umenukuu kwenye Mwaka

Shahidi (Tigo): Mwaka inatofautiana na Barua ya Polisi waliyoleta

Kibatala: Ni sahihi kwamba Jalada ulilonukuu wewe ni tofauti ambalo hata polisi wamekuletea

Shahidi (Tigo): Hapana

 

Kibatala: Ulitoa ufafanuzi wakati unaongozwa na wakili wa serikali kwamba umeulizwa barua kwa Jalada A wewe ukajibu Jalada B

Shahidi (Tigo): Hapana Sikusema

Kibatala: Twende eneo lingine, umetoa kielelezo namba P6 ni KYC. Nimesikia mnaulizana rekodi za NIDA Vs @Tigo_TZ Kwa kuwa Taarifa za Freeman Mbowe zipo NIDA, ni sahihi?

Shahidi: Ndiyo

 

Kibatala: kwa hiyo kimsingi NIDA ndiyo Primary Source za Freeman Mbowe

Shahidi: Haupo sahihi

Kibatala: Basi niambie Uhusiano wa Tigo na NIDA katika KYC

Shahidi (Tigo): Kwa sababu sisi tuna chukua Data Kwao kimtandao

Kibatala: Kwa hiyo utakubaliana na Mimi NIDA ni Primary Source

Shahidi (Tigo): Hapana

 

Kibatala: Usajili wa Tigo unaweza kutambulika bila Mtu Kusajiliwa NIDA

Shahidi (Tigo): Hapana

Kibatala: katika Ushahidi wako umezungumzia Lolote Kuhusu wewe Kusomea Mambo ya Data za NIDA

Shahidi (Tigo): Hapana Sikuzungumzia

Kibatala: Wewe unaweza Kuzungumzia suala la Server ya NIDA Kama siyo Administrator wa NIDA

Shahidi (Tigo): Hapana

 

Kibatala: Kuna aina Ngapi za Server

Shahidi (Tigo): Email Based, Data Based Server

Kibatala: Nikisema LINU server unaelewa

Shahidi (Tigo): Ndiyo naifahamu

Kibatala: Ni nini

 

Shahidi (Tigo): Maelezo yake sifahamu

Kibatala: Ni Lenox au Linux

Shahidi (Tigo): Linux

Kibatala: huku Taja Window Server

Shahidi (Tigo): Sikusema

Kibatala: SQL Server Foft ware

Shahidi (Tigo): Fost ware

 

Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama Server ni Software au Hardware

Shahidi (Tigo): Hard Ware

Kibatala: Kuna Version kadhaa za SQL Software

Shahidi (Tigo): Ndiyo

Kibatala tutajie The Latest SQL version

Shahidi (Tigo): Siwezi Kujua Kwa kweli

 

Kibatala: Sasa aliyemtajia Jaji Mambo ya SQL fotware ulilenga nini

Shahidi (Tigo): Kumuonyesha Jaji ni wapi nilipata Hizo Nyaraka

Kibatala: Wewe Hukutaka kabisa Jaji ajue Uimara, Uadilifu na Uimara wa hizo Software

Shahidi (Tigo): Sikumwambia

 

Kibatala: Je unajua The SQL Software 2019 ndiyo The best wewe utakataa?

Shahidi: SIWEZI KUJUA NDIYO MAANA NIMESEMA SIWEZI KUELEZEA HIYO

Kibatala: kwa Maelezo yako SQL Server Mnayotumia ni ya 2015

Shahidi: Nilisema ile ndiyo nilisoma Kozi ya introduction, tume update juzi

Kibatala: Ulimwambia Jaji Kwamba Umeupdate Juzi

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

 

Kibatala: VAPT ni nini

Shahidi: NI Watu wakujaribu Umadhubuti wa mifumo

Kibatala: Kutokana na Umuhimu huo ndiyo Maana Mkawafuata Ernest & Young Taasisi Kubwa, Mmechukua Kwa ajili ya Ulinzi wa Mifumo?

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Kibatala: Sasa ulimwambia Mheshimiwa Jaji..?

 

Shahidi (Tigo): Siku Mwambia Exactly

Kibatala: Hatuna Kumwambia Exactly Wanasheria

Kibatala: Unafahamu DB2 software

Shahidi (Tigo): Siifahamu

 

Kibatala: Kwa hiyo wewe nikikwambia DB2 ndiyo madhubuti duniani kwa uwezo wake, huwezi kujua?

Shahidi (Tigo): Siwezi Kujua Kwa kweli

Kibatala: Na Unajua Kuwa SQL ni Moja software ya Bei Rahisi Duniani

Shahidi (Tigo): Inayoweza Kununulika (affordable)

Kibatala: Unafahamu Kwamba Tigo ni Reportimg Institution

Shahidi (Tigo): Ndiyo

 

Martin Maranja Masese @IAMartin_ · 48m Kibatala: Mlishawahi Ku’ report Mambo yasiyofahaa Kuhusu Hiyo namba za simu

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Kibatala: Unafahamu Kuwa PEGASUS ni SoftWare Hatari sana Duniani Kwa ajili ya Kuingilia Mawasiliano wa mtu

Shahidi (Tigo): Hilo sifahamu

Kibatala: Makao Makuu ya Tigo yapo Karibu kabisa na Eneo la Usalama wa Taifa

Shahidi (Tigo): Ndiyo

 

Kibatala: Unafahamu Kuna Pesa Za Mteja Zimeibwa Kwenye huduma ya Kibubu ya tigo, Na Mwanasheria Pacience Mlowe ameleta Demand Notes kwenu

Shahidi (Tigo): Hapana Sifahamu

Kibatala: Nakupeleka Kwenye Detail ya Miamala ya pesa

Kibatala: Kuna Originating Number na Terminating Namba

Shahidi (Tigo): Ndiyo

 

Kibatala: Wewe Ulionyeshwa hapa Mahakamani Kwamba hii Ndiyo Terminating Namba.?

Shahidi (Tigo): Sikuonyeshwa

Kibatala: unafahamu kuwa kuna Huduma ya Kurudisha Miamala

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Kwa hiyo hatuwezi Kusema Details za kuanzia Tarehe 01.8.2020 kama tunazo hapa

Shahidi: Ndiyo

 

Kibatala: Kwa hiyo hatujui Kama Pesa hiyo huenda mbele Ilirudishwa, Si Ndiyo

Shahidi:Ndiyo Hatujui

Kibatala kamaliza kuuliza maswali ya Dodoso.. Anasimama sasa Wakili wa Serikali Kwa ajili ya Re examination..

WS : Nitakuuliza Kwa ufafanuzi na Pole Kwa Maswali..

Leave a Comment