×

Majaliwa: Tanzania Kuendeleza Uhusiano Kimataifa

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kuwa Tanzania itaendeleza uhusiano na mataifa mbalimbali duniani ikiwemo Nchi ya Marekani katika sekta zote za maendeleo ili kusaidia kuongeza fursa za uwekezaji na biashara.

 

Ameyasema hayo leo (Jumatano, Februari 23, 2022) alipozungumza na wabunge wa Bunge la Marekani Katika ofisi ndogo ya Waziri Mkuu, Magogoni Jijini Dar es Salaam. Waziri Mkuu amesema kuwa wabunge hao wamefurahi kuona mahusiano kati ya nchi hizi mbili yanakua.

“Mahusiano yetu kiuchumi yanaendelea kuimarika, wanatambua mchango wa Tanzania katika kutoa fursa za uwekezaji hapa Tanzania na sisi kufanya nao biashara, tutaendelea kuimarisha kwa kuwa na ‘forum’ mbalimbali za wafanyabishara wa ndani ya Nchi na Wamarekani.”

 

Ameongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuendelea kuifungua Tanzania kimataifa katika maeneo mbalimbali ili kuongeza fursa kwa Watanzania.

Leave a Comment