×

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Alivyozindua Mbio za Kili Marathon Leo

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (katikati) alivyoshiriki Kilimanjari Marathon leo.

 

 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, jana Jumapili amezindua mbio za Kilimanjaro Marathon zilizoanzia Uwanja wa Chuo cha Ushirika Mjini Moshi.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alivyomaliza mbio za kilometa 5.

 

 

Baada ya uzinduzi huo Waziri Majaliwa alishiriki mbio za kilometa 5 na kuzimalizia kwenye uwanja huo.

Katika mbio hizo Aloyce Simbu wa hapa nchini Tanzania aliibuka mshindi wa kwanza huku wanawake Shelmith Muriuki kutoka Kenya ndiye aliyeibuka kidedea.

Waziri Mkuu akiwapongeza wakimbiaji wengine mara baada ya kuzindua mbio za kilometa 21 Tigo Marathon.

 

Wakimbiaji wa kilometa 42 wakianza kutifuana.

 

Katika mbio hizo kulukiwa na wakimbiaji wa kilometa 5 ambazo zinadhaminiwa na Grand Malt, kilometa 21 zinazodhaminiwa na Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi ya  Tigo na kilometa 42 ambazo zinadhamniniwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.                                       HABARI/PICHA NA RICHARD BUKOS /GPL

Leave a Comment