
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemkuta na kesi ya kujibu Mtangazaji wa Clouds FM, Mwemba Burton maarufu kwa jina la Mwijaku katika shtaka la kusambaza picha za utupu kinyume cha Sheria.
Ni baada ya Serikali kufunga ushahidi wao wa mashahidi watano na vielelezo vinne walivyoviwasilisha wakati wa ushahidi.
Mwijaku anashutumiwa kusambaza picha za utupu za Msanii wa Bongo Movie, Menina Alegria kati ya Septemba 17, 2019 na Oktoba 2019