×

Amref Yasisitiza Umuhimu wa Kupata Chanjo Ya Uviko-19

Timu ya Amref Tanzania ikitoa elimu ya UVIKO 19 Mkoani Simiyu

MKURUGENZI MKUU  wa Program ya  Kudhibiti na kuzuia magonjwa Amref Health Africa Tanzania Dkt.Rita Mutayoba amesema kuwa  Tanzania kwa ufadhili wa Africa CDC kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Ofisi ya Rais TAMISEMI na Kamati za Afya Mikoa ya Simiyu na Tanga  katika kutekeleza mradi wa chanjo ya UVIKO-19 unaolenga kuharakisha  upatikanaji wa chanjo kwa wananchi  katika Mikoa ya  hiyo Amref inatoa  elimu na kuhamasisha  jamii kutumia chanjo ya UVIKO-19 kwa kutumia mbinu  mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutumia mitandao ya jamii ambapo  matarajio yetu ni  kufikia wananchi wengi iwezekanavyo na taarifa sahihi kuhusu chanjo ya UVIKO-19 na kuongeza mwamko wa wananchi kutumia chanjo hii.

 

Katika kuendeleza jitihada za Serikali mwaka huu Shirika la Amref Health Africa Tanzania limeamua kufanya kampeni ambayo itachangia katika kusambaza elimu na hivyo kutoa hamasa kwa wananchi kupata chanjo ya UVIKO 19 huku lengo kuu likiwa kuisaidia serikali kufikia lengo la asilimia 70 ya watu wote wanaostahili kuchanja ifikapo Desemba mwaka huu.

 

“Kampeni hii inalenga kupeleka elimu kwa watanzania wote  ambao wanastahili kupata chanjo kundi  hili ni la watanzania wote wenye umri kuanzia miaka 18 na kuendelea”.

Kampeni hii inahusisha pia wahamasishaji wa mitandaoni ambao wamekuwa na ushawishi mkubwa katika masuala mbalimbali ya jamii.

Timu ya UVIKO19 ikitoa elimu kwa wananchi

Wahamasishaji hawa hutumia kurasa zao mitandaoni kwa kuweka taarifa sahihi juu ya  chanjo pamoja  na UVIKO 19.

 

Taarifa hizi hupitiwa na Wizara ya Afya kabla ya kuwekwa mitandaoni zimekuwa msaada mkubwa kwa wale wanaozipokea.

Leave a Comment