Rais Samia Awasili Zanzibar Baada ya Kuhitimisha Ziara Yake Nchini Oman na Saudi Arabia
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewasili Visiwani Zanzibar mara baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi nchini Oman pamoja na Saudi Arabia.
Rais Samia akiwa nchini humo alifanikiwa kuhudhuria Kongamano la mkutano na wafanyabiashara wa Oman pamoja na wale Tanzania ambapo aliongelea juu ya kuimarishwa kwa mahusiano na mazingira mazuri ya biashara baina ya mataifa hayo, huku akibainisha kuwa yeye kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atahakikisha anatengeneza mazingira mazuri ya wafanyabiashara kuwekeza nchini na wale wa Tanzania kuangalia fursa za nini cha kufanya katika mataifa hayo.