
Klabu ya Yanga imethibitisha kumrejesha mshambuliaji Tuisila Kisinda (22) raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo klabuni baada ya kuachana na klabu ya RS Berkane.
Kupitia mtandao wa Kijamii wa Instagram, Mwenyekiti wa Yanga, Hersi Said ameonekana akifanya maongezi mafupi na Kisinda kuashiria kuwa mchezaji huyo raia wa DR Congo amerejea nyumbani kwa mara nyingine.