×

Rais Samia Afungua Mkutano Mkuu Wa 10 Chama Cha Taaluma Ya Menejimenti – Video

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi pamoja na Wanachama wa Chama cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA) kabla ya kufungua Mkutano wa 10 wa Chama hicho uliofanyika kwenye ukumbi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) tarehe 27 Novemba, 2022.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan leo Novemba 27, 2022 amefungua Mkutano Mkuu wa Kumi wa Chama cha Taaluma ya Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania ( TRAMPA) katika Ukumbi wa AICC, ARUSHA.

Wanachama wa Chama cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA) pamoja na Wageni wengine wakimsikiliza mgeni Rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati akiwahutubia kabla ya kufungua Mkutano wa 10 wa Chama hicho uliofanyika kwenye ukumbi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) tarehe 27 Novemba, 2022.
Rais Samia akiwa na viongozi wa Chama cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka Tanzania (TRAMPA) katika picha ya pamoja na Wanachama wa Chama hicho mara baada ya kufungua Mkutano wa 10 wa Chama hicho uliofanyika kwenye ukumbi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) tarehe 27 Novemba, 2022.
Rais Samia akitoa Tuzo ya Heshima kwa wadau mbalimbali kutokana na michango yao katika kada ya uwekaji wa Kumbukumbu na nyaraka mara baada ya kufungua Mkutano wa 10 wa Chama cha Menejimenti na Kumbukumbuku na Nyaraka Tanzania uliofanyika kwenye ukumbi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) tarehe 27 Novemba, 2022.


Leave a Comment