
Dar es Salaam, 17 Agosti 2023: Ikiwa ni mwendelezo wa kampeni ya chawote ya kampuni ya tigo mpaka sasa imefikia zaidi ya washindi elfu kumi na saba.
Hayo ameyasema Mary Audax Rutta Meneja wa Wateja Maalum Tigo Pesa leo Agosti 18,2023 wakati akikabidhi hundi ya shilingi milioni moja kwa washindi hao Jijini Dar es Salaam iliyoshuhudiwa na waandishi wa habari.

Kwa upande wake Joyce Massaba Mkazi wa Dar es Salaam ambaye ni mshindi wa milioni moja amesema fedha hizo zitamsaidia kwenye malengo ya kibiashara anayotarajia kuyafanya.
Nae Amina Rajabu Mkazi wa Dar es salaam mshindi wa milioni moja ameongezea kwa kusema fedha hiyo itamsaidia kwenye biashara yake ya mama lishe kuongezea mtaji wake na kukuza biashara hiyo.

Sanjari na hayo mshindi mwingine wa milioni moja, Godfrey Tarimo mkazi wa Dar es Salaam amesema hela hiyo itamsaidia katika mambo yake mengine binafsi.
Promosheni hiyo ya chawote itadumu kwa siku tisini hii ikiwa ni wiki ya nane mshindi wa mwisho wa mwezi anashinda milioni tano mbali na zawadi za fedha taslim wanazotoa nyingine ni bonus, dakika na sms.