Klabu za Jogging zilivyokutana Dar Live leo
Timu ya mpira wa netiboli ikiwa kwenye pozi.
Mratibu wa klabu za jogging, Rajabu Mteta akizungumza jambo.
Meneja wa Dar Live, Juma Mbizo(mwenye kofia) akizungumza jambo na Mbunge wa Mbagala, Issa Mangungu.
…Akitazama risala.
Mbunge akijiandaa kufungua mashindano ya netiboli.
Baadhi ya klabu za jogging zilizo jitokeza katika Uwanja wa Dar Live.
Wanamichezo wakifuatilia jambo.
Klabu ya Kongowe Jogging ambao ndio waandaaji wakiwa kwenye pozi.
Klabu ya Kongowe Jogging kupitia mwenyekiti wake, Mshauri Balandu, leo imezindua kikundi cha vikoba katika umoja huo, uzinduzi na harakati hizo zilizohudhuriwa na klabu mbalimbali kutoka Jimbo la Mbagala na sehemu zingine za Jiji la Dar, zimefanyika kuanzia uwanja wa mpira wa Kongowe mpaka Viwanja vya Dar Live.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo ni Mbunge wa Jimbo la Mbagala, Issa Mangungu ambapo ameupongeza umoja huo, pia ametoa sh. laki tatu kama mchango wa kuiendeleza Kongowe Jogging, pia ameahidi kuwapatia viti 50 na kuzifungulia akaunti klabu zote za jimbo lake.
Jongging hiyo ilipambwa na michenzo mbalimbali ikiwemo, mpira wa miguu, netiboli, kudance, kuimba na mingineyo.
(Habari/Picha: Gabriel Ng’osha)