
Jubilee Health Insurance imetoa taarifa kuhusu mafanikio iliyoyapata katika Tanzania Service Excellence Awards (TSEA) 2025.
Taarifa hiyo inasoma kama ifuatavyo:
Jubilee Health Insurance inayo furaha kutangaza mafanikio yake makubwa katika Tanzania Service Excellence Awards (TSEA) 2025, iliyo fanyika Ijumaa, tarehe 28 Machi 2025.
Tuzo hii inatufanya tuongeze juhudi katika kutoa huduma bora kwa wateja, jambo ambalo limekuwa kipaumbele chetu kila wakati. Tunajivunia sana kupata tuzo hii ya heshima, ambayo inadhihirisha kazi ngumu ya timu yetu na imani kubwa ambayo wateja wetu wanayo kwetu.
“Tuzo hii ni heshima kubwa kwetu,” alisema Veronica Nyage, Mkuu wa Idara ya Kudumisha Wateja na Uzoefu wa Wateja katika Jubilee Health Insurance.
“Tuzo hii inaonyesha jitihada na kujitolea kwa timu yetu yote, na tumejizatiti kuendelea kuboresha huduma zetu kwa wateja wetu.”
Jubilee Health Insurance itaendelea kuzingatia kuridhika kwa wateja na ubora wa huduma, ikijivunia mafanikio haya na kuhakikisha huduma za afya bora zaidi kwa Watanzania.
Asante kwa wateja wetu, washirika, na wafanyakazi wetu kwa msaada wao usio na kikomo. Tunatarajia kufikia mafanikio makubwa zaidi pamoja!