The House of Favourite Newspapers
gunners X

Amiri Jeshi Mkuu Rais Samia Afungua Mkutano wa 9 wa Mkuu wa Majeshi Tanga – Video

0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. Samia akizungumza na Wakuu wa Kamandi, Wakuu wa Matawi na Makamanda wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kabla ya kufungua mkutano wa 9 wa Mkuu wa Majeshi na Makamanda uliofanyika katika Shule ya Kijeshi ya Ulinzi wa Anga (SKUA) mkoani Tanga tarehe 15 Desemba 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu,  Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewasili katika Shule ya Kijeshi ya Ulinzi wa Anga (SKUA), mkoani Tanga, leo Desemba 15, 2025, kwa ajili ya ufunguzi wa Mkutano wa 9 wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Makamanda.

Mkutano huu unalenga kuimarisha ushirikiano wa kijeshi, kuboresha mikakati ya ulinzi wa taifa, na kuchambua changamoto na mafanikio ya jeshi katika kuhakikisha usalama wa nchi na raia wake.

Rais Samia amekuwa mstari wa mbele katika kuhimiza ufanisi na uwajibikaji katika majeshi, huku akisisitiza umuhimu wa kuendeleza mafunzo bora, ujasiri, na nidhamu miongoni mwa maofisa na askari wa Tanzania.

Matukio mbalimbali wakati wa Mkutano wa 9 wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Makamanda uliofanyika katika Shule ya Kijeshi ya Ulinzi wa Anga (SKUA) mkoani Tanga. Mkutano huo wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Makamanda ulifunguliwa na rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, tarehe 15 Desemba, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika Shule ya Kijeshi ya Ulinzi wa Anga (SKUA) mkoani Tanga kwa ajili ya kufungua mkutano wa 9 wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Makamanda, tarehe 15 Desemba, 2025.

 

Leave A Reply