Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, akizungumza na washiriki wa kikao kazibaina ya OSHA na Maafisa Biashara wa Mikoa na Wilaya za Kanda ya Kaskazini(hawapo pichani).
Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) umezindua mpango wake wakushirikiana na Maafisa Biashara wa Mikoa na Wilaya katika kuwezesha biashara nauwekezaji nchini.
Mpango huo unahusisha utaratibu wa kuunganisha mifumo na kubadilishana taarifa za biashara na miradi mbalimbali ya uwekezaji ili kurahisisha ufikishaji wa huduma za urasimishaji biashara na ukaguzi wa mifumo ya usalama na afya mahali pa kazi.
Meneja wa Usalama Mahali pa Kazi wa OSHA, Mhandisi Robert Mashinji, akiwasilishamada kuhusu usajili wa maeneo ya kazi na utekelezaji wa majukumu ya OSHA kwaujumla katika kikao kazi baina ya OSHA na Maafisa Biashara wa Mikoa na Wilaya za Kanda ya Kaskazini.
Bi.Mwenda amesema mpango huo umeibuliwa ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye amekuwa akielekeza Taasisi za serikalikushirikiana katika utendaji ikiwemo kuhakikisha kwamba mifumo mbalimbali ya serikaliinasomana.
“Lengo kuu la mpango huu ni kuhakikisha kuwa Taasisi ya OSHA inafanya kazi kwakushirikiana na wenzetu ambao ni Maafisa Biashara wa Mikoa na Wilaya wote tukiwakama Taasisi wezeshi katika biashara na uwekezaji,” ameeleza Mtendaji Mkuu waOSHA na kuongeza:
“Tumekuwa na kikao kizuri sana ambacho kimetufungulia zoezi letu ambalo tumepangakulifanya nchi nzima. Mpango huu utakapokamilika sote tutakuwa na uelewa wa pamojaambao utapelekea taasisi zetu kuwa wawezeshaji zaidi badala ya kuwa wadhibiti washughuli za biashara na uwekezaji nchini.”
Kwa upande wao washiriki wa semina hiyo ambao ni Maafisa Biashara wa Mikoa naWilaya zote za Kanda ya Kaskazini ikihusisha mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga, wamepongeza mpango huo na kuahidi kushirikiana na OSHA kufanikishampango huo.
Washiriki wa kikao kazi baina ya OSHA na Maafisa Biashara wa Mikoa na Wilaya za Kanda ya Kaskazini wakifuatilia mawasilisho toka kwa wataalam wa OSHA kuhusuSheria na Usalama na Afya Mahali pa Kazi pamoja na utekelezaji wa majukumu yaOSHA kwa ujumla.
“Tumefurahia sana mafunzo ya leo,hakika tumetoka na ufahamu mpana kuhusiana nakazi za OSHA na tumeona kuna umuhimu mkubwa sana kwa wafanyabiashara nawawekezaji kujisajili katika mfumo rasmi ili waweze kuweka salama sehemu zao za kazi,” ameeleza Bw. Elisha Erasto, Mkuu wa Idara ya Biashara wa Halmashauri yaWilaya ya Rombo.
“Tunaishukuru sana OSHA kwa semina ya leo na kwaniaba ya washiriki wenzanguninapenda kusema kwamba tutashirikiana na OSHA ili kufanikisha mpango huuunaolenga kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini na hivyo kufanikishamalengo ya Dira ya Taifa 2050,” amesema Bi. Lulu Kaaya, Afisa Biashara Mkoa waArusha.




