×

Trump Awasiliana na Wanaanga wa Artemis II “Mmeifanya Marekani Kujivunia” – Video

Wanaanga wa Artemis II wakizungumza na Rais Donald Trump kutoka ndani ya Orion spacecraft siku ya Jumatatu.

Rais wa Marekani Donald Trump amewapigia simu wanaanga wa misheni ya Artemis II masaa machache baada ya kufanikisha safari yao ya kihistoria kuzunguka upande wa mbali wa mwezi.

Safari hiyo imeweka rekodi mpya, huku wanaanga hao wakifika umbali mkubwa zaidi kutoka duniani kuliko binadamu yeyote katika historia ya anga.

Katika mazungumzo hayo, Trump aliwapongeza kwa mafanikio yao makubwa, akisema:
“Mmeandika historia na mmeifanya Marekani kujivunia sana.”

Pia alitambua mchango wa mwanaanga kutoka Canada, Jeremy Hansen, ambaye ni sehemu ya timu hiyo ya kimataifa.

Misheni ya Artemis II inaonekana kuwa hatua muhimu kuelekea malengo ya kurejesha binadamu mwezini, ikiwa ni maandalizi ya safari zijazo zitakazohusisha kutua rasmi kwenye uso wa mwezi.

Leave a Comment