×

Makonda Afichua Mpango wa Kuwaleta Mike Tyson na Floyd Mayweather Jr. Tanzania

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema yapo mazungumzo yanaendelea ili kuwaleta nchini mabondia Mike Tyson na Floyd Mayweather.

Makonda amesema hayo Mei 1, 2026 wakati akizungumza kwenye msimu wa nane wa pambano la ngumi la Vita ya Kisasi (Knockout ya Mama) ambapo, Bondia Assemahle Wellem ametetea ubingwa wake wa WBO Afrika kwa TKO ya raundi ya nne dhidi ya Prince Oko Nartey.

Assemahle Wellem ni raia wa Afrika Kusini ambaye kwa sasa anaishi nchini na ana leseni ya Tanzania.

Leave a Comment