×

Trump Atangaza Kumalizika kwa Vita na Iran Bungeni Marekani – Video

Rais wa Marekani, Donald Trump, ametangaza mbele ya Bunge la Marekani kuwa vita na Iran ‘vimekwisha’, huku akisisitiza kuwa hana nia ya kuondoa vikosi vyake eneo hilo kwa haraka.

Rais huyo pia amejaribu kuimarisha hoja yake kwamba hahitaji idhini ya wabunge kuendelea na operesheni hiyo ya kijeshi.

Katika barua aliyowasilisha kwa viongozi wa Bunge Ijumaa, Mei 1, wakati ukikaribia mwisho wa muda wa kuwasilisha taarifa kuhusu vita hivyo, Trump alisema hakuna mapigano yoyote yaliyotokea kati ya pande hizo mbili tangu kusitishwa kwa mapigano.

Ameiambia Congress kuwa ‘mapigano yaliyoanza Februari 28, 2026 yamemalizika.’

Leave a Comment