
Mashabiki wa usiku wa kuamkia leo Mei 20, 2022 wamejaa kwenye baa, vilabu na mitaa mbalimbali kusherehekea ubingwa baada ya miaka 22 huku wengine wakionekana wakikumbatiana, kuimba nyimbo za timu na hata kupanda juu ya meza kutokana na furaha kubwa waliyoipata.
Baadhi ya maeneo yaliyokuwa na shamrashamra kubwa ni pamoja na baa maarufu za mashabiki wa Arsenal kama World’s End iliyopo Finsbury Park pamoja na The Tollington iliyopo karibu na uwanja wa.

Hata hivyo, huenda hakuna aliyefurahia ushindi huo kama gwiji wa klabu,, mwenye umri wa miaka 62, ambaye aliitumikia Arsenal kwa mafanikio makubwa na kufunga mabao 185 akiwa klabuni hapo.
Legenda huyo alivumilia kipindi chote cha miaka 22 bila ubingwa wa Premier League pamoja na mashabiki wengine wa Arsenal, lakini safari hiyo iliisha kwa furaha kubwa huku akiwa katikati ya mashabiki waliokuwa wakishangilia kwenye mitaa ya Kaskazini mwa London.









