
Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) wanakaribisha maombi kutoka kwa Watanzania wenye sifa stahiki kujaza nafasi mbalimbali za ajira za mkataba wa mwaka mmoja.
Taasisi hii ni chuo cha umma kilicho chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara kinachojihusisha na ufundishaji, utafiti na ushauri wa kitaalamu katika fani za biashara na taaluma zinazohusiana.
NAFASI ZILIZOPO
1. Msaidizi wa Maktaba Daraja la II – Nafasi 5
Sifa:
- Shahada ya Sayansi ya Maktaba au fani zinazofanana
Majukumu:
- Utafutaji wa taarifa za maktaba
- Kuhudumia wasomaji
- Usajili wa watumiaji
- Kutoa na kupokea vitabu
2. Msaidizi wa Maktaba – Nafasi 3
Sifa:
- Cheti cha Maktaba na Taarifa au sawa na hicho
Majukumu:
- Huduma za maktaba
- Usajili wa wasomaji
- Kushughulikia maulizo rahisi
- Kutoa na kupokea vitabu
3. Afisa Majengo II (Uhandisi wa Ujenzi) – Nafasi 1
Sifa:
- Shahada ya Uhandisi wa Ujenzi
- Usajili kama Graduate Engineer
Majukumu:
- Matengenezo ya majengo
- Kuandaa bajeti na ratiba za kazi
- Usimamizi wa mazingira ya chuo
4. Afisa Majengo II (Usanifu Majengo) – Nafasi 1
Sifa:
- Shahada ya Usanifu Majengo
- Usajili kama Graduate Architect
Majukumu:
- Matengenezo ya majengo
- Upangaji wa miradi ya majengo
- Usimamizi wa mazingira ya chuo
MAOMBI YANAHITAJIKA KUJUMUISHA:
- CV kamili
- Vyeti vya elimu
- Cheti cha kuzaliwa
- NIDA
- Mawasiliano kamili (simu na anuani)
ANUANI YA MAOMBI:
The Rector
College of Business Education
S.L.P 1968
Dar es Salaam
MWISHO WA MAOMBI:
Ndani ya siku 14 kuanzia tarehe ya tangazo (18 Mei 2026)
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MKATABA CHUO CHA ELIMU YA BIASHARA (CBE) 18-05-2026