×

Mexico Yakubali Kuwa Mwenyeji wa Timu ya Iran Kombe la Dunia 2026 Kufuatia Mvutano na Marekani

Rais wa Mexico Claudia Sheinbaum ametangaza kuwa nchi hiyo itaihifadhi timu ya taifa ya Iran wakati wa mashindano ya 2026 FIFA World Cup baada ya Marekani kuonyesha kutotaka kuipokea kutokana na mvutano wa kisiasa unaoendelea.

Sheinbaum amesema kuwa FIFA iliwasiliana na serikali ya Mexico kuomba msaada huo baada ya utawala wa Rais Donald Trump kueleza kuwa si salama kwa timu ya Iran kuwepo Marekani.

“Hakuna sababu ya kuwanyima nafasi ya kukaa Mexico,” alisema Sheinbaum katika mkutano wake wa kila siku na waandishi wa habari.

Awali Iran ilikuwa imepangwa kucheza michezo yake yote ya hatua ya makundi nchini Marekani, lakini sasa timu hiyo inapanga kuhamishia kambi yake kutoka Tucson, Arizona kwenda Tijuana karibu na mpaka wa Marekani.

Rais wa Shirikisho la Soka la Iran, Mehdi Taj, alithibitisha kuwa uamuzi huo ulifikiwa baada ya mazungumzo na viongozi wa FIFA mjini Istanbul pamoja na mkutano wa mtandao na Katibu Mkuu wa FIFA, Mattias Grafstrom.

Mvutano huo umechochewa na vita vinavyoendelea kati ya Marekani, Israel na Iran tangu Februari mwaka huu, hali iliyozua sintofahamu kuhusu ushiriki wa Iran kwenye mashindano hayo makubwa ya soka duniani.

Licha ya changamoto hizo, Iran imefanikiwa kufuzu kwa mara ya nne mfululizo kushiriki Kombe la Dunia na inabaki kuwa moja ya timu bora ndani ya Shirikisho la Soka Asia.

Katika ratiba ya mashindano, Iran inatarajiwa kucheza dhidi ya New Zealand mjini Los Angeles Juni 15, kabla ya kukutana na Belgium Juni 21 na baadaye Egypt mjini Seattle Juni 26 kwenye kundi G la michuano hiyo.

CCM NA CHADEMA BADO NGOMA NGUMU/MWANASHERIA ANAFUNGUKA TUME YA KIJINAI/BURIANI MAMA MAGUFULI

Leave a Comment