×

Kombe la Dunia Lapamba Moto, Mechi Mbili Kubwa Kuteka Hisia za Mashabiki leo

Nyasi kuwaka moto leo kwenye mechi za michuano mikubwa Duniani ambapo mataifa makubwa uanatarajiwa kushuka dimbani kuoneshana mbavu. Je nani kufurahia mwisho wa Kimpyenga cha mwamuzi?

Majira ya saa 5:00 usiku kutakuwa na mechi ya kibabe kati ya Uholanzi dhidi ya  Japan huku huu ukitarajiwa kuwa moja ya mchezo wenye ushindani mkubwa kutokana na uwezo wa timu zote mbili kucheza soka la kasi na lenye mpangilio mzuri. Uholanzi wanaingia wakiwa na faida ya uzoefu mkubwa katika mashindano makubwa na kikosi chenye ubora wa kiufundi, jambo linalowafanya kuwa miongoni mwa timu zinazotegemewa kufanya vizuri katika mashindano haya. Beti sasa.

Japan wao wamekuwa wakionyesha maendeleo makubwa katika miaka ya hivi karibuni na wamejijengea sifa ya kuwa timu yenye nidhamu, kasi na uwezo mkubwa wa kucheza kwa pamoja. Wajapani wanaweza kuwasumbua Uholanzi kupitia mashambulizi ya haraka na uwezo wao wa kubadilika haraka kutoka ulinzi kwenda kushambulia.

Huu unatarajiwa kuwa mchezo wa ushindani mkubwa katikati ya uwanja, huku timu zote zikihitaji kuwa makini ili kuepuka kufanya makosa yatakayoweza kuamua matokeo. Uholanzi wanaonekana kuwa na ubora mdogo kutokana na uzoefu wao, lakini Japan wana uwezo wa kufanya mchezo huu kuwa mgumu na hata kusababisha mshangao.

Jishindi mkwanja kwa haraka kwenye michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile Keno, Aviator, Poker, Roullette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.

Kundi E, kitawaka haswa kati ya Ujerumani dhidi ya Curaçao huku wajerumani wakitaka kuanza kampeni yao kwa nguvu na kuonyesha ubora wao dhidi ya timu inayoshiriki mashindano haya ikiwa na ari kubwa ya kufanya vizuri.

Ujerumani wanaingia wakiwa na kikosi chenye uzoefu mkubwa na uwezo wa kutawala mchezo kupitia umiliki wa mpira na mashambulizi ya haraka, huku wakitarajia kutumia ubora wao wa kiufundi kuvunja safu ya ulinzi ya wapinzani wao wakiwemo Musiala, Gnabry, Havertz, Kimmich na wengine wengi.

Huku timu hii ya Curaçao, hii ni mechi ya kihistoria na nafasi ya kujipima dhidi ya moja ya mataifa makubwa zaidi katika soka la dunia. Watahitaji kucheza kwa nidhamu kubwa na kutumia vizuri nafasi chache watakazopata ikiwa wanataka kuleta ushindani dhidi ya Wajerumani.

Je Curacao wanaweza kuwazuia mabingwa hawa wa 2014 kuanza bila ushindi?. Tandika jamvi kwenye mechi hii sasa.

Leave a Comment