×

G7 Yarejea Kujadili Vita vya Ukraine Baada ya Mgogoro wa Iran

Mke wa Rais wa Uswisi, Caroline Merotto, Waziri Mkuu wa Japan, Sanae Takaichi, Rais wa Uswisi, Guy Parmelin, Mke wa Rais wa Brazil, Rosangela ‘Janja’ da Silva, Rais wa Brazil, Luiz Inácio Lula da Silva, Rais wa Korea Kusini, Lee Jae-myung, Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, Mke wa Rais wa Korea Kusini, Kim Hye-kyung, Mke wa Rais wa Ufaransa, Brigitte Macron, Mke wa Waziri Mkuu wa Uingereza, Victoria Starmer, Rais wa Marekani, Donald Trump, Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi, Waziri Mkuu wa Canada, Mark Carney, Mke wa Waziri Mkuu wa Canada, Diana Carney, Rais wa European Commission, Ursula von der Leyen, Mke wa Kansela wa Ujerumani, Charlotte Merz, mume wa Ursula von der Leyen, Heiko von der Leyen, pamoja na Kansela wa Ujerumani, Friedrich Merz, wakipiga picha ya pamoja kabla ya chakula cha jioni cha viongozi kama sehemu ya Mkutano wa G7 Summit uliofanyika mjini Evian-les-Bains tarehe 16 Juni 2026.

Donald Trump amesema Marekani inaweza kurejesha vikwazo dhidi ya usafirishaji wa mafuta ya Russia katika siku za karibu, huku viongozi wa mataifa ya G7 wakielekeza tena nguvu zao katika vita vya Ukraine baada ya mgogoro wa Iran kupungua.

Akizungumza katika mkutano wa G7 uliofanyika mjini Evian-les-Bains, Trump alisema hatua ya kulegeza baadhi ya vikwazo vya mafuta ya Urusi iliyochukuliwa miezi iliyopita ililenga kusaidia kudhibiti bei ya mafuta duniani wakati wa mgogoro wa Ghuba, lakini sasa inaweza kufutwa kutokana na kurejea kwa usafirishaji wa mafuta kupitia Hormuz.

“Sasa mafuta yanaendelea kusafirishwa, hivyo hivi karibuni tutakuwa katika nafasi ya kurejesha vikwazo hivyo,” alisema Trump.

Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy, alishiriki mazungumzo na viongozi wa G7 kuhusu hali ya vita nchini mwake. Baada ya kikao hicho, Zelenskyy alisema mataifa yote ya G7 yanaendelea kuunga mkono Ukraine katika juhudi zake za kujilinda dhidi ya uvamizi wa Urusi.

Aliongeza kuwa viongozi hao walijadili kuongeza upatikanaji na uzalishaji wa makombora ya ulinzi ya Patriot, ambayo yamekuwa muhimu katika kuzuia mashambulizi ya makombora ya Urusi dhidi ya miji na miundombinu ya Ukraine.

Wakati mkutano huo ukiendelea, Urusi iliripotiwa kufanya mashambulizi makubwa ya ndege zisizo na rubani na makombora dhidi ya miji mikubwa ya Ukraine, mashambulizi yaliyosababisha vifo vya watu kadhaa na uharibifu wa miundombinu.

Vita kati ya Urusi na Ukraine sasa vinaendelea kwa zaidi ya miaka minne tangu uvamizi kamili wa Urusi ulipoanza, huku juhudi za kufikia amani zikiendelea kukumbana na changamoto.

Mbali na suala la Ukraine, Trump pia alizungumzia makubaliano ya kusitisha mzozo kati ya Marekani na Iran, akisema yuko tayari kuyawasilisha mbele ya Bunge la Marekani kwa ajili ya mapitio.

Aidha, alionesha kutoridhishwa na jinsi Israel inavyoendelea kushughulikia mzozo wake na kundi la Hezbollah nchini Lebanon, akisema hali hiyo inaweza kuathiri juhudi za kuimarisha amani katika eneo hilo.

Leave a Comment