
Spain wana mfumo thabiti wa umiliki na udhibiti wa mpira, huku wachezaji wao wakiwa wamekua katika falsafa moja ya kimuundo toka ngazi za chini. Kwa upande mwingine, Portugal wanategemea vipaji vya mtu mmoja mmoja na ubunifu wa washambuliaji wao wa ubavuni kama Rafael Leão na Pedro Neto, ambao ndio hatari kubwa zaidi kuliko hata Cristiano Ronaldo mwenyewe kwa sasa.
Kipa wa Spain, Unai Simon, ameonya dhidi ya kumdharau Ronaldo, akisema “Cristiano tunayemwona sasa si yule wa miaka sita au saba iliyopita, lakini lazima umweke mbali na eneo la penalti”. Hata hivyo, kocha wa Portugal Roberto Martinez alimuondoa Ronaldo dakika ya 82 dhidi ya Kroatia, na Goncalo Ramos akafunga bao la ushindi, jambo linalozua maswali kuhusu kama ni wakati wa kuanza na kizazi kipya.
Moja ya vita kuu itakuwa ubavuni kati ya Lamine Yamal wa Spain na Nuno Mendes wa Portugal. Yamal amekuwa hatari sana, hasa anapopokea mpira na nafasi nyuma ya mlinzi wake. Mendes anakabiliwa na mtanziko: kuendelea kuvamia mbele kusaidia mashambulizi au kujitolea kikamilifu kwa ulinzi dhidi ya Yamal. Kwenye mchezo uliopita ubavu wa kushoto wa Portugal ulikuwa udhaifu dhidi ya Kroatia, na iwapo wataruhusu Yamal nafasi, Spain wanaweza kufunga.
Ingia kwenye kasi ya kujishindia pesa kwenye michezo ya Kasino ya Mtandaoni kama vile, Keno, Aviator, Poker, Roulette, Wild Icy Fruits, Super Heli na mingine kibao. Jiunge leo kwa kutembelea tovuti ya meridianbet.co.tz au piga *149*10# kisha uanze safari yako ya ushindi.
Katika kiungo, ni pambano kati ya nyota wa PSG na kikosi cha Spain kilichokomaa zaidi. Vitinha na Joao Neves wa Portugal wanacheza pamoja kila siku PSG na wana uelewano mzuri, lakini kiungo cha Spain cha Rodri, Pedri, na Dani Olmo kimeonyesha umaridadi zaidi katika mashindano haya.
Spain kama timu iliyo na nafasi kubwa. Wameshamaliza mechi nne bila kufungwa bao, wakiwa na rekodi ya dakika 519 bila kuruhusu bao rekodi mpya ya mashindano ya Dunia. Mshambuliaji Mikel Oyarzabal amefunga mabao 17 katika mechi 16 za mwisho akiwa kwenye kikosi cha kwanza. Hata hivyo, mechi za kuondoa mara nyingi huamuliwa na makosa madogo, na Portugal wana uwezo wa kuchukua nafasi zao.