
ZANZIBAR: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amempokea Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Félix Antoine Tshisekedi Tshilombo, katika Ikulu Ndogo ya Zanzibar leo, tarehe 18 Agosti 2026.
Rais Tshisekedi aliwasili Zanzibar na kupokelewa na Rais Samia katika ziara inayosisitiza uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mapokezi hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali, huku Rais Samia na Rais Tshisekedi wakibadilishana salamu kabla ya kuendelea na shughuli zao za kikazi.
Ziara hiyo inatarajiwa kuendelea kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na ushirikiano kati ya mataifa hayo mawili katika maeneo mbalimbali yenye maslahi ya pamoja.
