
Mtangazaji wa Global TV Online na 255 Global Radio, Zali Mapito, yupo nchini Oman kufuatilia hali ya binti mdogo wa Kitanzania, Neema Kengele, kutoka Geita, ambaye amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) kwa siku kadhaa.
Akizungumza akiwa Oman katika mahojiano na mtangazaji God Muya wa Global TV, Zali ameeleza kwa kina hali inavyoendelea pamoja na juhudi zinazofanyika kuhakikisha Neema anapata msaada unaohitajika.
Katika maelezo yake, Zali amebainisha pia juhudi zinazofanywa na Balozi wa Tanzania nchini Oman, Maulidah Hassan, katika kufuatilia na kusaidia katika suala hilo.
Ujio wa Zali nchini Oman unalenga kufuatilia kwa karibu maendeleo ya hali ya Neema pamoja na kupata taarifa sahihi kuhusu hatua zinazochukuliwa na mamlaka pamoja na wahusika mbalimbali katika kuhakikisha Mtanzania huyo anapata matibabu na msaada unaohitajika.
Hali ya Neema imeendelea kufuatiliwa kwa karibu, huku Watanzania wakisubiri taarifa zaidi kuhusu maendeleo yake.