×

Ajira Mpya 678 Zatangazwa Serikalini, Madaktari na Walimu Watajwa

Dodoma, Septemba 3, 2026 — Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (PSRS), kwa niaba ya

Tangazo hilo lenye Kumb. Na. JA.9/16/01/56, limetolewa Septemba 3, 2026, likiwa na nafasi katika kada mbalimbali kuanzia madaktari, wauguzi, walimu, wataalamu wa mifugo hadi watumishi wa ofisi.

Nafasi zilizotangazwa

1. Daktari Daraja la II – Nafasi 115

Waombaji wanatakiwa kuwa na Shahada ya Udaktari kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali, wawe wamekamilisha mafunzo ya Internship na kupata usajili kutoka Baraza la Madaktari Tanganyika.

Majukumu yanahusisha kutoa huduma za matibabu, elimu ya afya, kuzuia milipuko ya magonjwa, kutunza takwimu za afya, kusimamia watumishi na kushiriki katika kuboresha ubora wa huduma za afya.

Mshahara: TGHS E

2. Afisa Muuguzi Msaidizi Daraja la II – Nafasi 128

Nafasi hizi ni kwa wenye Stashahada ya Uuguzi ya muda usiopungua miaka miwili kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali.

Mwombaji anatakiwa pia kuwa amesajiliwa na Baraza la Wauguzi na Wakunga Tanzania.

Mshahara: TGHS B3. Afisa Mifugo Daraja la II – Nafasi 39

Waombaji wanatakiwa kuwa na Shahada ya Sayansi ya Wanyama (Animal Science) au Shahada ya Sayansi ya Kilimo aliyebobea katika Sayansi ya Wanyama kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine au sifa inayolingana kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali.

Majukumu yanahusisha kupanga na kusimamia uzalishaji wa mifugo, kutoa mafunzo kwa wafugaji, kuratibu miradi ya mifugo, kukusanya takwimu na kushiriki katika kudhibiti changamoto zinazohusiana na mifugo na mazingira.

Mshahara: TGS D

4. Tabibu wa Kinywa na Meno Daraja la II – Nafasi 17

Waombaji wanatakiwa kuwa na Stashahada ya Tabibu wa Meno (Diploma in Clinical Dentistry) kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali na wawe wamesajiliwa na Baraza la Madaktari.

Mshahara: TGHS B

5. Mteknolojia Maabara Daraja la II – Nafasi 25

Nafasi hizi ni kwa wenye Stashahada katika Uteknolojia wa Maabara za Afya kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali.

Mwombaji anatakiwa pia kuwa amesajiliwa na Baraza la Wataalamu wa Maabara.

Mshahara: TGHS B

6. Mwandishi Mwendesha Ofisi Daraja la II – Nafasi 74

Waombaji wanatakiwa kuwa na elimu ya Kidato cha Nne au Kidato cha Sita, pamoja na Stashahada ya Uhazili (NTA Level 6).

Wanapaswa pia kuwa wamefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza kwa kasi ya maneno 100 kwa dakika moja na kuwa na ujuzi wa programu za kompyuta za ofisi kama Word, Excel, PowerPoint, Internet, E-mail na Publisher.

Mshahara: TGS C

7. Mwalimu Daraja la III C – Fizikia – Nafasi 55

Waombaji wanatakiwa kuwa na Shahada ya Elimu/Bachelor of Education yenye somo la Fizikia au shahada isiyo ya ualimu yenye Fizikia kama somo la kufundishia pamoja na Stashahada ya Uzamili ya Elimu (PGDE).

Mshahara: TGTS D

8. Mwalimu Daraja la III C – Hisabati – Nafasi 67

Waombaji wanatakiwa kuwa na Shahada ya Elimu/Bachelor of Education yenye Hisabati kama somo la kufundishia, au shahada isiyo ya ualimu yenye Hisabati pamoja na PGDE.

Mshahara: TGTS D

9. Mwalimu Daraja la III B – Fizikia – Nafasi 43

Nafasi hizi ni kwa wahitimu wenye Cheti cha Kidato cha Sita waliofaulu masomo mawili au zaidi yanayofundishwa shuleni na wenye Stashahada ya Ualimu ya miaka miwili yenye Fizikia kama somo la kufundishia.

Mshahara: TGTS C

10. Mwalimu Daraja la III B – Hisabati – Nafasi 48

Waombaji wanatakiwa kuwa na Cheti cha Kidato cha Sita, wakiwa wamefaulu masomo mawili au zaidi yanayofundishwa shuleni, pamoja na Stashahada ya Ualimu ya miaka miwili yenye Hisabati kama somo la kufundishia.

Mshahara: TGTS C

11. Afisa Misitu Msaidizi Daraja la II – Nafasi 28

Waombaji wanatakiwa kuwa na Stashahada katika fani kama Forestry, Agroforestry, Forest Resources Assessment and Management, Forest Biology, Forest Economics, Forest Engineering au fani inayohusiana.

Majukumu ni pamoja na kusimamia ukusanyaji wa mbegu na bustani za miti, kukusanya takwimu za misitu, kusimamia upandaji na utunzaji wa miti, kupima mazao ya misitu na kufanya doria.

Mshahara: TGS C

12. Afisa Afya Mazingira Msaidizi Daraja la II – Nafasi 26

Waombaji wanatakiwa kuwa na Stashahada ya Sayansi ya Afya ya Mazingira kutoka chuo kinachotambuliwa na Serikali na wawe wamesajiliwa na Bodi ya Wataalamu wa Afya Mazingira.

Majukumu yanahusisha kudhibiti milipuko ya magonjwa, kutoa elimu ya afya ya mazingira, kukagua usalama wa maeneo ya chakula, kusimamia sheria za afya ya mazingira na kuhamasisha jamii kuhusu usafi na afya.

Mshahara: TGHS B

13. Mwalimu Daraja la III C – Fasihi ya Kiingereza – Nafasi 13

Waombaji wanatakiwa kuwa na Shahada ya Elimu/Bachelor of Education yenye Fasihi ya Kiingereza kama somo la kufundishia, au shahada isiyo ya ualimu yenye somo hilo pamoja na PGDE.

Mshahara: TGTS D

Masharti muhimu ya maombi

Waombaji wote wanatakiwa kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wasizidi umri wa miaka 45.

Waombaji wenye ulemavu wanahamasishwa kutuma maombi na wanapaswa kuainisha aina ya ulemavu wao kwenye mfumo wa maombi.

Mwombaji anatakiwa kuambatisha cheti cha kuzaliwa kilichothibitishwa na Mwanasheria/Wakili, pamoja na vyeti vya elimu na vyeti vya kitaaluma vinavyohitajika kwa nafasi husika.

Sekretarieti ya Ajira imesisitiza kuwa Testimonials, Provisional Results, Statement of Results pamoja na Result Slips za Kidato cha Nne na Kidato cha Sita hazitakubaliwa.

Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wanapaswa kuhakikisha vyeti vyao vimethibitishwa na mamlaka husika kama TCU, NECTA au NACTVET, kulingana na sifa husika.

Aidha, waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa wawe na kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.

Mwisho wa kutuma maombi

Mwisho wa kutuma maombi ya nafasi hizi ni Septemba 17, 2026.

Maombi yote yanatakiwa kutumwa kwa njia ya kielektroniki kupitia Recruitment Portal ya Sekretarieti ya Ajira.

Barua ya maombi iliyosainiwa inapaswa kuambatishwa pamoja na vyeti vinavyohitajika na ielekezwe kwa:

KATIBU,
OFISI YA RAIS,
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA,
Mtaa wa Mahakama, Tambukareli,
S.L.P. 2320,
DODOMA.

Sekretarieti ya Ajira imeonya kuwa maombi yatakayowasilishwa nje ya utaratibu uliowekwa hayatafikiriwa.

Aidha, waombaji wamekumbushwa kuwa ni marufuku kutoa au kupokea rushwa kwa lengo la kupata ajira au kupangiwa kituo cha kazi. Mchakato wa ajira unapaswa kuzingatia misingi ya haki, usawa na uwazi.

Limetolewa na:
KATIBU
SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

Leave a Comment