
Shahidi wa nne wa upande wa utetezi katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, Brenda Rupia, amekamilisha kutoa ushahidi wake leo Septemba 9, 2026.
Rupia, ambaye ni Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA, amekuwa akijibu maswali ya mawakili wa Serikali kuhusu hotuba mbalimbali za Lissu, ikiwemo kauli zinazodaiwa kuwa na maneno kama “tutahamasisha uasi”, “hakuna reforms, hakuna uchaguzi” na “tutakinukisha.”
Katika dodoso hilo, Wakili wa Serikali, Katuga, alimuuliza Rupia kuhusu video ya Lissu aliyosema aliiona kupitia YouTube ya Jambo TV. Shahidi alithibitisha kuiona video hiyo, akisema Lissu alikuwa amevaa vazi la combat, ingawa hakukumbuka rangi ya vazi hilo wala kama alikuwa amevaa miwani.
Rupia pia alikiri kuwa katika video hiyo kulikuwa na bendera ya Taifa, huku alipoulizwa kuhusu bendera ya CHADEMA akisema hakumbuki na kuomba sehemu hiyo ya ushahidi ifutwe.
Katika sehemu nyingine ya ushahidi, Rupia alikiri kwamba Lissu alitumia neno “uasi”, lakini alieleza kuwa kwa uelewa wake kauli hiyo ililenga kupinga sheria kandamizi.

Alipoulizwa kuhusu kauli ya CHADEMA ya “No Reforms, No Election”, Rupia alisema ilikuwa ni msimamo wa chama uliomaanisha kuwa bila mabadiliko hakutakuwa na uchaguzi, lakini akasisitiza kuwa chama hakikusema kingezuia uchaguzi.
Wakili Katuga pia alimuuliza shahidi kama Lissu alielekeza njia za kuvuruga uchaguzi au “kukinukisha”, ambapo Rupia alijibu kuwa alielekeza.
Kwa upande wake, Wakili Job alimuuliza Rupia kuhusu majukumu yake kama Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA. Shahidi alieleza kuwa moja ya majukumu yake ni kuratibu mawasiliano ya chama na umma kupitia vyombo vya habari, pamoja na kusimamia utendaji wa watu walio chini ya idara yake.
Rupia pia alieleza kuwa ana elimu ya Accounting na hakusomea uandishi wa habari, lakini akasisitiza kuwa anasimamia idara nzima ya mawasiliano ya chama.
Katika maswali ya Wakili Tawabu Issa Tawabu, Rupia alisisitiza kuwa kwa mtazamo wake Lissu hakufanya kosa, huku akisema mamlaka ya mwisho ya kuamua kama mtu ametenda kosa ni mahakama.
Alipoulizwa maana ya uhaini, Rupia alisema kwa uelewa wake ni kuisaliti nchi au kutaka kupindua serikali. Kuhusu uasi, alitoa tafsiri kuwa ni kitendo cha kikundi cha watu kupinga au kubadili mfumo wa nchi bila kufuata sheria.
Wakili Tawabu pia alimuuliza kuhusu umiliki wa maudhui yaliyotangazwa na Jambo TV. Rupia alisema maudhui hayo ni mali ya chombo husika cha habari na kwamba Lissu si mmiliki wa Jambo TV wala maudhui hayo.
Wakati wa maswali ya Wakili Cuthbert Mbiling’i, Rupia alikiri kuwa yeye ni kiongozi wa CHADEMA na kwamba amekuwa mwanachama wa chama hicho tangu mwaka 2013. Alikubali pia kuwa ushahidi anaoutoa ni wa kumtetea kiongozi wake, lakini akasema yeye ni “shahidi mwenye interest ya haki kutendeka”, si kwa sababu ya kumlinda Lissu bila kujali ukweli.
Rupia pia alithibitisha kuwa Lissu alitamka maneno “uasi” na “tutakinukisha”, lakini akasisitiza kuwa maneno hayo hayakuwa kosa kwa uelewa wake.
Katika maswali ya Wakili Winniwa, shahidi alieleza tafsiri yake ya neno “uasi” kuwa ni kupinga au kukataa kwa nguvu kubwa. Alipoulizwa maana ya “kukinikisha”, alisema linahusiana na kitu kunukia au kunuka vibaya, akitoa mfano wa mtu anayepika pilau na harufu yake kuwafanya wengine watambue kuwa kuna mtu anapika.
Baada ya mawakili wa Serikali kukamilisha maswali yao, Jaji alitangaza kuahirisha mwenendo wa kesi hadi kesho saa 3:00 asubuhi, huku upande wa utetezi ukiendelea na hatua zake katika kesi hiyo.
Shahidi wa tano wa upande wa utetezi anatarajiwa kuendelea na ushahidi katika hatua inayofuata ya kesi hiyo.
Baada ya kukamilika kwa hatua hiyo, majaji waliiahirisha kesi hiyo kwa muda wa saa moja na nusu, hadi saa 8:30 mchana, ambapo shahidi wa tano wa upande wa utetezi anatarajiwa kupanda kizimbani kuanza kutoa ushahidi katika kumtetea Lissu.
-
Katuga: Waambie majaji kama ulifanikiwa kuona video ya mwemyekiti kwenye mtandao wa youtube wa jambo Tv.
Brenda: Ndio nilifanikiwa kuiona.
Katuga: Mshtakiwa alikuwa ameonekana amevaa nini?
Brenda: Nguo za Chama Combat
Katuga: Alikuwa amevaa combat ya rangi gani?
Brenda: Sikumbuki.
Katuga: Alikuwa amevaa miwani?
Brenda: Sikumbuki
Katuga: Ni kweli kwamba ndani ya kombat alikuwa amevaa tshirt nyeusi?
Brenda:Sikumbuki
Katuga: Kama uliona hiyo video kwenye nyuma kulikuwa na bendera ya taifa na chama.
Brenda: Ndio ni kweli kulikuwa bendera ya taifa na chadema.
Katuga: Bendera ya Chadema ina rangi gani?
Brenda: Blue, nyeupe na nyekundu
Katuga: Waambie majaji kama unakumbuka mashahidi waliosema wameona hii video na unakumbuka ushahidi wao wakisema walimuona mwenyekiti akiwa amevaa miwani, kombat na nyuma yake kuna bendera ya taifa na chadema.
Brenda: Sikumbuki
Katuga: Hawa mashahidi waliambia mahakama walimuona lissu amevaa kombat sasa wewe na hawa mashahidi nani alisema uongo
Brenda: Sikumbuki.
Katuga: Unajua vitu vingine ni virahisi kama hawa mashahidi wamesema kwamba alikuwa amevaa kombat na nyuma yake kuna bendera.
Brenda: Ni ushahidi wangu kwamba mwenyekiti alikuwa amesimama nyuma kuna bendera ya taifa ila kama kuna bendera ya chadema sikumbuki naomba mfute hiyo.
Katuga: Waambie majaji kama ulisikia akisema majaji ni maccm.
Brenda: Sikumbuki.
Katuga: Waambie majaji kama alisema mahakamani hakuendeki.
Brenda: Sikumbuki
Katuga: Waambie majaji kama ukisikia watafanyaje watatuua si watanikamata na kunifungulia kesi ya uhaini?
Brenda: Ndio
Katuga: Wakati unamsikia mwenyekiti akisema atashtakiwa kwa uhaini hii kesi ilikuwa imefunguliwa?
Brenda: Hapana
Katuga: Una mamlaka gani kusema kesi hii ni ya uongo?
Brenda: Mahakama ndio ina mamlaka kisheria Mimi sina mamlaka
Katuga: Ulisikia akisema mapolisi wanaingia na kura feki kwenye vibegi mgongoni.
Brenda:Nilimsikia.
Katuga: Unajua kama mshtakiwa ana kesi ya kutoa taarifa uongo Kisutu?
Brenda: Sifahamu
Katuga: Yaani hufahamu ?
Brenda: Naomba nikumbushe kama yapo.
Katuga: Waambie majaji kama mwenyekiti hakutaka hotuba yake ifikie umma.
Brenda: Sijui kama alitaka au hakutaka.
Katuga: Waeleze majaji kama unajua mh lissu ana vyombo vyake binafsi vya kutoa taarifa zake.
Brenda: Sijui kama ana vyombo binafsi.
Katuga: Waambie majaji wakati mwenyekiti anataka kutoa taarifa yake kwa umma huwa anafanya nini kuufikia umma?
Brenda: Sijui.
Katuga:Unajua au hujui kwamba mwenyekiti akitaka taarifa ifike kwa umma anaongea na waandishi wa habari.
Brenda: Anafanya press conference.
Katuga: Kwa hiyo ni ushahidi wako kwamba bwana mshtakiwa njia pekee anayotumia kuchapisha taarifa yake kwa wananchi ni kupitia vyombo vya habari.
Katuga: Neno uasi lazima lielekezwe dhidi ya watu fulani.
Brenda: Ni dhidi ya mtu watu fulani ni sahihi.
Katuga: Waambie majaji hili neno tutahamasisha uasi ambalo unasema ulisikia mwenyekiti akilisema ilikua kuhamasisha uasi dhidi ya nani?
Brenda: Dhidi ya sheria kandamizi.
Katuga: Sasa waambie majaji ile kuhamasisha uasi dhidi ya sheria ilikuwa ni kuichana hii sheria.
Brenda: Dhidi ya sheria kandamizi.
Katuga umezitaja.
Brenda: Sijataja naomba nizitaje waheshimiwa majaji.
Katuga: Hivi mabadiliko ya kisiasa yanafanywa na watu au taratibu za kisheria.
Brenda: Nguvu na mamlaka ni ya watu hivyo watu ndio wanafanya mabadiliko.
Katuga: Uasi unaenda dhidi ya mfumo na watu wenye mamlaka au dhidi ya sheria kandamizi.
Katuga: Aliposema tutahamasisha uasi waambie waheshimiwa mtazuia sheria zisifanye uchaguzi au mtazuia watu.
Brenda: Yalilenga sheria kubadilishwa.
Katuga: Waambie majaji kwamba sheria ndio zinashiriki kupiga kura.
Brenda: Hapana.
Katuga: Unaenda kuzuia watu wasipige kura au sheria.
Brenda: Sheria.
Katuga: Nani wanapiga kura?
Brenda: Watu wanapiga kura.
Katuga: Unapozuia uchaguzi unamanisha nini unazuia watu au?
Brenda: Unazuia mchakato mzima.
Katuga: Unajua au hujui kama chadema inaamini katika demokrasia
Brenda: Iko kwenye falsafa ya chama.
Katuga: Unajua Tanzania iko katika mfumo wa vyama vingi?
Brenda: Ndio.
Katuga: Waambie majaji kama hii no reforms no election ilikuwa katika msimamo wa chama.
Brenda: Ndio
Katuga: Kuna ushahidi hapa mahakamani kwamba no reforms no election ni msimamo uliolenga kuzuia uchaguzi mpaka mabadiliko yafanyike.
Brenda: Sio kweli ni msimamo wa chama hakuna mabadiliko hakuna uchaguzi.
Katuga: Niko sahihi kusema chadema ilimaanisha kama hakuna mabadiliko hakuna uchaguzi.
Brenda: ilisema hakuna mabadiliko hakuna uchaguzi haikusema itazuaia uchaguzi.
Katuga: Unafahamu uchaguzi upo kwa mujibu wa katiba?
Brenda: Nafahamu.
Katuga: Waambie majaji kama unafahamu kubadili katiba ni mchakato.Waambie majaji kwa kuwa wewe unatuambia katiba ni mchakato na uchaguzi uko kwa mujibu wa katiba mlioanza kusema kama hakuna mabadiliko hakuna uchaguzi na no reforms ilianza 2024.
Katuga: Iambie mahakama ilipanga vipi kuzuia uchaguzi katika hotuba yake.
Brenda: Alielekeza.
Katuga: Alielekeza njia za kuvuruga uchaguzi?
Brenda: Alielekeza.
Katuga: Alielekeza au hakuelekeza njia ya kukinukisha?
Brenda: Alielekeza.
-
Jaji: Tuendeleee
Katuga: Kwa jina langu nitakuwa sahihi nikisema wewe ni mnyawezi mwenzangu
Brenda: Ndio
Katuga: Waambie majaji kama ulikuepo siku ya kupiga kura na ulikua wapi
Brenda: Nilikuwepo nyumbani basi haya
Katuga: Una cheo gani kingine ndani ya chama?
Brenda: Mimi Katibu wa BAWCHA mkoa wa Kinondoni
Katuga: Waambie majaji kama ulikitaja cheo hicho
Brenda: ililenga mabadiliko katika nyanja ya kisiasa
Katuga: Waambie majaji kama katika hituba ya mwenyeki kama ni ushahidi wako kwamba uliona hiyo video
Brenda: Ni kweli niliona hii video
Katuga: Je, ni kweli uliona kwenye mtandao wa kijamii wa Jambo
Brenda: Ni ni kweli
Katuga: Uliangakia youtube ya Jambo TV
Brenda: Nimesema mitandao ya kijamii twende na hiyo hiyo youtube
Katuga: Waambie waheshimiwa majaji kama nikikusikia sahihi ukisema neno kukinukisha ni slang sio neno rasmi
Brenda: Ndio nilisema
Katuga: Nitakuwa sahihi nilisema slang ni lugha isiyo rasmi inayotumika na kundi kwenye jamii
Brenda: Ndio kama hivyo utakuwa sahihi
Katuga: Waambie majaji kama katika ushahidi wako ulisema maana yake na inatumika na kundi gani
Brenda: Sikusema inatumika na kundi gani nilisema maana yake
Kataga: Kama nitakuwa sahihi ulisema kukinukisha ni kufanya kitu kinukie vizuri au vibaya ni slan au lugha rasmi
Brenda: Ni tafsiri
Katuga: Kitendo cha kufanya kitu kinukie kinaitwaje
Brenda: Kukifanya kinukie
Katuga: Nitakuwa sahihi nikisema nimekinukisha
Brenda: Utakuwa sahihi
Katuga: Kwa kuwa hujataja ni kundi gani wanatumia hiyo slang nitakuwa sahahi nikisema inatumika na vijana wenu
Brenda: Utakuwa sahihi
Katuga: Nitakuwa sahihi nikisema mtu akisema anaenda kukinukisha anaenda kufanya jambo lisilo la kawaida
Brenda: Sijui
Jaji: hilo litakuwa swali la mwisho
Katuga: Ukisema raisi wa Jamuhuri ya Muungano hajatajwa kwenye hotuba ya mwenyekiti
Brenda: ndio
Katuga: Mheshimiwa jaji umenielekeza hilo ni swali la mwisho
Jaji: Tuna ahirisha mpaka kesho saa tatu asubuhi kesho tuwahi
Katuga: Kuna nyaraka mshitakiwa aliomba zimeshapitiwa naomba apokee
Lissu: Hawa watu wananipa nyaraka zangu kama kina nani sababu hawa ndio wananishitaki
Jaji: Kwa hiyo unazihitaji?
Lissu: Niliomba maana yake nazihitaji
Jaji: Naomba hizo nyaraka mshitakiwa apewe
Katuga: Nina maswali yasiyopungua hamsini na hayajirudii na nikiangalia ni saa kumi na moja kamili
Jiji: Wewe anza tunafidia dakika tano tulizopoteza asubuhi na tunafidia nusu saa tuliyopoteza asubuhi.
Job: Kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa kuna mahali sheria hiyo inaruhusu kuvuruga uchaguzi?
Brenda: Sijui
Job: Kwa kuwa kwenye majibu yako umeeleza mahakama unaunga mkono maneno yote yaliyoko kwenye hati ya mashitaka kitendo hicho ni ukiukwaji wa katiba ya Chadema
Brenda: Utakuwa hauko sawa
Job: Kwa lugha nyingine kama sio sahihi unawaeleza majaji swala la kuvuruga uchaguzi kukinukisha kama lilivyosemwa na mshitakiwa msingi wake ni ibara ya tatu tatu moja ya katiba ya chadema
Brenda: Wingi wake unatokana na msimamo wa chama
Brenda: Msingi wake unatokana na msimamo wa chama
Job: Msingi unatokana na ibara ya tatu moja tatu
Brenda: Ndio unatokana na ibara hiyo
Job: Umetoa tamko lolote kuhusiana na mwenendo wa kesi hii
Brenda: Sikumbuki
Job: Una shida ya kumbukumbu?
Brenda: Hapana nimetoa matamko mengi ila sio specific kwenye kesi hii licha ya kwamba nimekuwa nikitoa maoni yangu juu ya mwenyekiti kuendelea kushikiliwa sababu ya nia ovu ya serikali
Job:Ulitoa hayao kupitia wapi
Brenda: Kupitia simu yangu na mitandao ya kijamii
Job: Ulikuwa unazungumza na nani
Brenda: Ukiwa mtandaoni uzungumza mbele ya kamera ya simu yako
Job: ila ulitaka umma wa watanzania wafuatilie na wajue
Brenda: Ndio
Job: Ilikuwa lini
Brenda: Sikumbuki ilikuwa lini
Job: ilikuwa mwaka gani
Brenda: Kati ya mwaka huu na mwaka jana
Job: Una fahamu kutokujua sheria hakuondoi kosa
Brenda: Ndio
Job: Unafahamu jinai haifi
Brenda: ndio
Job: utakubaliana na mimi tamko hilo ulilotoa ni kinyume cha sheria za nchi
Brenda: Hapana
Job: Naomba nishie hapa wenzangu waendelee
Job: Shahidi nina maswali machache…Kama nilikusikia vyema ulishiriki kwenue ule mkutano wa tarehe tatu april 2025
Brenda: Ndio nilishiriki
Job: Nataka uwaambie majaji mwenyekiti wa chama Tundu Lissu wakati anaongea na hadhara alipotamka haya maneno uliyosomewa hapa aliungwa mkono hakuungwa mkono?
Brenda: Sijui
Job: Umeiambia mahakama ulikuepo
Brenda: Ndio nilikuepo
Job: Hebu iambie mahakama hii majukumu yako mahususi
Brenda: Ni pamoja kusimamia itifaki kwenye mikutano ya ndani na ya hadhara iwapo Katibu Mkuu anakuwa hayupo
Job: Swali linaweza kuwa pana tuliweke hivi kwenye hiyo sehemu ya mawasiliano kazi yako nini
Brenda: Waheshimiwa Majaji kuhusiana na mawasiliano huwa na ratibu pale chama kinapohitaji waandishi wa habari ambao kupitia kwao chama kinawasiliana na umma.Lakini pia mimi ninasimamia utendaji wa kazi unaofanywa na watu chini yangu
Job: nitakuwa sahihi nikisema wewe sio Afisa Mawasiliano ni afisa mualikaji
Brenda sio sahihi mimi nasimamia idara yote
Job: Watu walioko chini yako wanafanya nini kuhusiana na mawasiliano
Brenda: Wana alika waandisha wa habari wanawasiliana na viongozi wanawasiliana na umma kupitia vyombo vya habari. Wanataoa matangazo kwa niaba ya kurugenzi ya mawasiliano ya chama
Job: Kwa hicho ulivhosema ni sahihi kuwa moja ya jukumu lako ni kuhabarisha umma
Brenda: Ndio ni sahihi
Job: Utakubaliana na mimi kwamba moja ya sheria katika nchi hii inayosimamia maswala ya habari ni media service act
Brenda: Ndio
Job: Ukiwa kama mkurugenzi wa mawasiliano umesoma
Brenda: Ndio
Job: Inatumika na nani
Brenda: Watu walioko chini yangu
Job: Waambie majaji wewe umesoma nini
Brenda: Accounting
Job: Huna elimu kuhusiana na mambo ya habari na wewe sio mwandishi wa habari
Brenda: Hapana sijasomea uandishi wa habari
Job: Ndugu shahidi umewahi kusikia neno kishoka
Brenda: Sijawahi kusikia kwa kingereza ni nini
Job: Utakubaliana na mimi kwamba mtu yeyote anayefanya kazi ya kutoa huduma ya habari na hana sifa za kutoa hiyo kwa mujibu wa sheria anakiuka maadili ya habari?
Brenda: Sijui
Job: Ni sahihi unawaeleza majaji ukiwa unafanya kazi Chadema ya kuhabarisha umma huitaji kuwa na sifa zilizo ainishwa kwenye sheria kwamba yeyote yule sheria hii haimuhusu
Job: Sasa jibu swali
Brenda: Rudia swali
Job: Ni sahihi kwamba mtu yeyote ambaye hana sifa za kutoa huduma ya habari anaweza kufanya kazi kwenye idara ya mawasiliano Chadema?
Brenda: Sio sahihi
Job: Kama nimekusikia vizuri ukisema taaluma ya habari sio hitajio kwenye hiyo idara
Brenda: Sio sahihi
Job: Kama sio sahihi wewe ambaye unafanya kazi pale unafanya kazi kikamisa na hujui chochote
Brenda: Sio kweli kwamba sijui chochote na siko peke yangu niko na idara
Job: Nakuuliza wewe
Brenda: Sio sahahi relax Job
Brenda: Wewe ndo relax mbona unapata hasira ghafla
Job: Tukisema mtu asiye na sifa ya kutoa uandishi wa habari ni kanjanja
Brenda: Sifahamu
Job: Ni sahihi umekuwa mwanachama wa Chadema kwa muda sasa
Brenda: Ndio nimekuwa mwanachama tangu mwaka 2013
Job: Nitakuwa sahihi nikisema wewe …Brenda Rupia unaifahamu vyema Chadema
Brenda: Ndio
Job: Nini ni falsafa ya Chadema
Brenda: Chadema inaamini katika nguvu ya umma
Job: hiyo nguvu ya umma imetafsiriwa vipi kwenye katiba yenu
Brenda: Waheshimiwa majaji sio vizuri sana kukariri vifungu lakini ni kushirikisha umma mambo yake ikiwa chaguzi na kushirikisha umma katika matukio katika maamuzi
Job: Hayo unayofafanua yameandikwa kwenye katiba
Brenda: Ni tafsiri yangu mimi kama brenda
Job: Nitakuwa sahihi nikikuambia wewe Brenda huijui vyema falsafa ya Chadema?
Brenda: Utakua hauko sahihi
Job: Kwa sababu umepatia au nimekosea
Brenda: Utakua hauko sahihi
Job: Nitaomba shahidi atusomee ibara ya tatu ya chama chao niweze kumuuliza maswali
Brenda: Falsa ya chama ni kuamini katika nguvu ya umma
Job: Soma tatu moja tatu
Brenda: anasoma …………..
Job: Swali umeelewa sawa hiyo ibara
Brenda: Ndio nimeelewa
Job: Unaelewa kwamba nchi hii ina katiba
Job: Wewe kama Brenda ulimuunga mkono wakati anatamka yale maneno
Brenda: Ndio nilimuunga mkono
Job: Kwa kukubaliana naye
Brenda: Ninakubaliana naye na hata leo nakubaliana na hayo maneno
Job: Ni sahahi kwamba ibara ya tatu moja tatu inaelekeza Chadema kulinda katiba ya Tanzania
Brenda: Ni sahihi
Job: Na utakubaliana mimi sheria ya uchaguzi hapa nchini Tanzania ni moja ya sheria iliyotungwa katika msingi huu wa kikatiba
Brenda: Nakubaliana na wewe
Job: Katika msingi huo swala la kuvuruga uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka 2025 ni ukikwaji wa katiba ya nchi?
Brenda: Sijui
Job: Hebu isaidie mahakama waambie majaji kabla ya uchaguzi mkuu ufanyike ni sahihi kwamba Tume ya Uchaguzi imekuwa na utaratibu wa kutoa kanuni ya maadili ya wanasiasa yanayopaswa kuasainiwa
Brenda: Ni sahihi
Job: Wewe ukiwa kama mwenezi chadema ilisaini hizo kanuni mwaka 2020
Brenda: Sikumbuki
Tawabu: Uliposema ameshitakiwa kwa uongo unadanganya
Brenda: Shitaka ni la uongo
Tawabu: Imo au haimo kwamba alichapisha jambo
Brenda: Hilo halimo jambo tv haijatajwa kwenye hati ya mashitaka
Tawabu: Kuna watu uliwataja wako kwenye sekretarieti
Brenda: Sikumtaja John Heche kwenye sekretarieti
Tawabu: Ulisema maudhui ni mali ya chombo husika cha habari
Brenda: Nilisema mmliki wa maudhui ni chombo husika cha habari na. mmliki namba moja atakuwa mkurugenzi wa chombo husika
Tawabu: Diamond, Mbosso na Mario una wafahamu?
Brenda: Nawasikia
Tawabu: Wanajihusisha na nini?
Brenda: Ni wanamuziki
Tawabu: Kwa hiyo anachokisema Tundu Lissu kupitia Jambo TV sio cha kwake?
Brenda: Ndio sio cha kwake
Tawabu: Uliulizwa haya maneno yaliyoko kwenye hati ya mashitaka ni kosa sio kosa
Brenda: Sio kosa
Tawabu: Unakumbuka tafsiri ya uasi nakuopa kamusi utusomee tena
Brenda: Kitendo cha kuwapinga wenye mamlaka..Kitendo cha uvunjaji wa sheria kinachofanywa na kikundi cha watu wanaotaka kuziondoa mamlaka za nchi yao
Tawabu: Kwenye maneno ya huyu bwana neno uasi lilikuwpo halikuepo
Brenda: Lilikuepo
Tawabu: Ulisema kwamba kufanya kitu kitoe harufu nzuri au mbaya sio kosa
Brenda: Sio kosa
Tawabu: Ukifuga kuku wakatia harufu mbaya sio kosa au ni kosa
Brenda: Sioni kama nin kosa waheshimiwa Majaji
Tawabu: Kuna kifungu kwenye pino kodi kinaongelea kutoa harufu mbaya je huoni unakinzanza na sheria
Brenda: Mimi sijui nifafanulie hiyo sheria
Tawabu: Nikikuambia kuna sheria inazuia watu wasitoe harufu mbaya utakubaliana na mimi
Brenda: Nisomee hiyo sheria mimi siwezi kukubali
Tawabu: Wewe ni mtaalamu wa hesabu
Brenda: Nimesomea account
Tawabu: Mtu akisema asilimia ina maanisha nini
Brenda: Ndio
Tawabu: Ukisema asilimia kubwa una maanisha nini
Brenda: Ni zaidi ya asilimia hamsini
Tawabu: Na hukufafanua
Brenda: Ndio sikufafanua
Tawabu: Hawa zaidi ya asilimia hamsini ni wakina nani
Brenda: siwakumbuki
Tawabu: Kuna mahala ulisema tarehe kumi mwezi wa sita kwengine tarehe 17 ulikuwa unatumia kalenda gani
Brenda: Nilikuwa ninamaanisha tarehe niliyoitaja
Tawabu: Ulikuwa unamaanisha aina gani ya kalenda
Brenda: Sijui aina ya kalenda
Tawabu: Ulipokuwa unatoa ushahdi ulirudia sana mwenyekiti wa chama mkurugenzi wa chama hapa Tanzania kuna vyama vingapi vya kisiasa
Brenda: Nasikia viko 19
Tawabu: Unaweza kututajia hata viwili
Brenda: Chadema, ACT, Chauma
Tawabu: Ulikuwa unasema mkuregenzi wa chama na hukusema chama gani
Brenda: Waheshimiwa Majaji nilipoanza kujieleza nilisema mimi ni Mkurugenzi Mawasiliano na Uenezi Chadema
Tawabu: unakubali kwamba ulisema chama ila hukussema chama gani
Brenda: Ndio
Tawabu: Umetuambia wewe ni mkurugenzi wa mawasiliano na uenezi
Brenda: Ndio
Tawabu: Unaposema mshitakiwa sio mfanyakazi wa Jambo TV kwa nafasi yako unaweza kujua?
Brenda: Hapana siwezi kujua
Tawabu: Umetuambia kwamba neno uasi ilitokana na kauli ya G55 hao G55 waliongea wakati gani kwenye mkutano wenu
Brenda: Hawakuongea alikuwa anajibu waraka wao
Tawabu: Unakubaliana na mimi mahakama hii ni ya kisheria na sio kihisia
Brenda: Ndio ninakubalina
Tawabu: Ulisema umekamatwa na polisi lakini haujawahi kupelekwa mahakamani hivyo unaombaia mahakama uko tayari kama mambo yako yamekubalika
Brenda: Kama wanaona kama wanamashitaka niko tayari
Tawabu: Ni hayo tu waheshia majaji
Tawabu Issa Tawabu: Naomba utusomeee neno haki kwenye kamusi
Brenda: anasoma ……..
Tawabu: Kwa hiyo hapo kamusi inasema haki ni kumpa mtu kile anachostahili
Brenda: Hiyo ni definitation moja
Tawabu: Huyu mwamba anashitakiwa kwa kukika kifungu cha 39 cha kanuni ya adhabu hiyo nakupa taarifa sasa kanuni ya adhabu ni sheria na mahakama inasimamia haki na hilo lipo kikatiba.
Brenda: Ndio
Tawabu: Uliposema huyu bwana hajatenda makosa ulitoa wapi hayo mamlaka ya kusema hivyo
Brenda: Mamlaka ndio yenye kauli ya mwisho
Tawabu: Wewe hayo mamlaka unayo
Brenda: Mamlaka ya kutoa kauli ya mwisho ni ya mahakama
Tawabu: Umeulizwa sana kuhusu maneno aliyosema mshitakiwa umewahi kuelewa maana ya uhaini ni nini
Brenda: Ni kuisaliti nchi yako kutaka kupindua serikali huo ndio uelewa wangu wa uhaini
Tawabu: Kwa kuwa umetuambia tafsiri yako ya uhaini kwa uelewa wako wa kawaida na kukiwa na tafsiri nyingine inayoweza kuthibitishwa na Mahakama na mtu akatendewa haki huna shida.
Brenda: Ndio
Tawabu: Umeulizwa sana kuhusu uasi kamusi ya kiswahili inasemaje kuhusu uasi
Brenda: Kitendo kinachofanywa na kikundi cha watu kubadili mfumo wa nchi yao bila kufuata sheria
Tawabu: Hivyo ni sahihi tafsiri ya uasi ndio hiyo
Brenda: Nitaenda na B
Tawabu: Kwa hiyo uasi ni kuvunja sheria
Brenda: Ni sahihi kwa moja ya fasiri
Tawabu: Nchi yetu ni ya kisheria au inaendeshwa kiimla
Brenda: kiimla
Tawabu: Na kinachofanyika hapa Mahakamani
Brenda: Haya ni ya kimahakama
Tawabu: Uliambia mahakama una uwezo wa kufanya miujiza
Brenda: Hapana
Tawabu: Uliposema ulipanda gari halina milango ulioandaje
Brenda: Hiyo humaan error
Tawabu: kwahiyo unedanganya
Brenda: Hapana magari ya mapolisi yako wazi
Tawabu: Uliposafirishwa na pro boxx uliwekwa wapi
Brenda: Nyuma
Tawabu: Walikutesa sana
Brenda: Sijasema
Tawabu: Nyuma ulikaa upande gani
Brenda: Nyuma Kushoto
Tawabu: Mlikuwa watu wangapi
Brenda: Watu watatu Jaji kwa maana ya wasijulikana wawili
Brenda: Ndio mheshimiwa Jaji
Tawabu: Nitakuwa sawa sawa nikisema ushahdi uliotoa hauhusiani na kesi hii
Brenda: Sijui
Tawabu: Hati yako ya kusafiria ina husiana na kesi ya mwenyekiti ya kukinukisha?
Brenda: Ilikuwa ni mwendelezo wakuonesha namna namna watawala wanavyokandamiza viongozi wa Chadema
Tawabu: Jibu swali
Brenda: Nareja ni mwelezo wa ukandamizaji
Tawabu: Kuna sehemu passport yako imeandikwa tutahamasisha uasi
Brenda: Nimesema ni mwendelezo wa ukandamizaji. wa raia
Tawabu: Uongo ni nini
Brenda: Mwenyekiti sio mhaini shitaka lake ni la uongo
Tawabu: Kwa mujibu sheria shitaka lipo au lipo.
Brenda: Shitaka ni la uongo.
Cuthbert Mbiling’i: Yale maneno ya kwenye hati ya mashitaka hayana ubishani kwamba alisema mwenyekiti
Brenda: Ni kweli aliyasema
Cuthbert: Mi kweli alisema uasi
Brenda: Alisema
Cuthbert: Tutakinukisha
Brenda: Tutakinukisha kweli kweli
Cuthbert: Unafahamu anashitakiwa na nini
Brenda: Hayo maneno kuwa ni uasi
Cuthbert: Umesema hayo sio makosa
Brenda: Ndio sio makosa
Cuthbert: Waambie majaji kwa mujibu wa sheria ipi
Brenda: Sijui kuhusu sheria
Cuthbert: Waambie majaji hayo ni maoni
Brenda: Ni fact
Cuthbert: Ulikamatwa Namanga na hukuIambia Mahakama ulikamatwa kwanini
Brenda: Waliniambia ni sababu ya taarifa niliyotoa
Cuthbert: Unajua kwamba jinai haiozi
Brenda: Nafahamu
Cuthbert: Kwa hiyo wakitaka kukupeleka mahakamani
Brenda: Wakiona inafaa
Cuthbert: Umesema ulikamatwa na mtu mwingine
Brenda: Nilikamatwa na nilimuona leonard magere mahabusu
Cuthbert: Taarifa ya kukamatwa kwako umeileta mahakamani
Brenda: Hapana
Cuthbert: Tangu unajiunga Chadema una miaka zaidi ya kumi. Je nafasi uliyo nayo muhusika anapatikanaje
Brenda: Nimejiunga Chadema mwaka 2013 na nimeshika nafasi mbali mbali na kumteua mkurugenzi wa mawasiliano kuna mchakato wa kikatiba unafuatwa
Cuthbert: Na huwezi kuchaguliwa kama sio mwanachama wa Chadema
Brenda: Ni sahihi
Cuthbert: Unafahamu nani alikupendekeza
Brenda: Sifahamu
Cuthbert: Unakubaliana na mimi kwamba ni mmoja wa viongozi wa chama
Brenda: Ndio
Cuthbert: na utakubaliana mimi utendaji wako wa kazi unarIpoti kwa katibu mkuu na viongozi wengine wajuu
Brenda: Ninatoa taarifa kwa sekretarieti ya Chama
Cuthbert: Unapofanya nakisa ya kiutumishi unawajibishwa na nani?
Brenda: Kamati kuu
Cuthbert: Na ni sahihi kwamba 20/8/2026 kamati kuu walikaa kikao
Brenda: Ndio sikumbuki tarehe lakini ila ni juzi juzi tu hapa
Cuthbert: Na moja kati ya maazimio ya kikao ilikuwa kumtetea mwenyekiti kwa nguvu mahakamani
Brenda: Sio shahihi
Cuthbert: Akitokea mtu mwingine akasema hivyo nani atakuwa maeidanganya mahakama
Brenda: Huyo mtu mwingine atakuwa amaeidianganya mahakama Cuthbert: Ni wajibu wako kufata maelekezo ya viongozi wako wa chama
Brenda: Ni sahihi
Cuthbert: Ulishwahi kutoa ushahidi wowote dhidi ya kiongozi yeyete wa Chadema dhidi yake sio kumetetea
Brenda: Sijawahi
Cuthbert: Na kuhusu kumtetea mwanachama au kiongizi wa chama mahakamani?
Brenda: Hii ndio mara ya kwanza Cuthbert na nikisema wewe ni shahidi mwenye interest sio shahidi huru
Brenda: Mimi ni shahdi mwenye interest ya haki kutendeka
Cuthbert: Utakubaliana na mimi ushahidi wako uchukuliwe kwa tahadhari sababu una interest
Brenda: Sijui
Cuthbert: Jana ukisema mshitakiwa sio mmiliki wa jambo tv wala hizo content zilizorushwa
Brenda: Ndio
Cuthbert: Una ushahidi wa kuthibitisha hilo
Brenda: Sijaleta waheshimiwa majaji
Cuthbert: Waheshimiwa majiji naomba niishie hapo.
Winniwa: Maana ya kuvuruga uchaguzi umesema sio kosa
Brenda: Sio kosa
Winniwa: Unafahamu uchaguzi uko kisheria
Brenda: Uchaguzi huru na wa haki
Winniw: Chaguzi zote ziko kisheria
Brenda: Ziko kwa mujibu wa sheria
Winniwa: Je mtu akitaka kuvuruga uchaguzi anavunja sheria
Brenda: Sio kweli
Winniwa: Sawa kwa uelewa wako lakini
Winniwa: Ulisema ulikuwa unaenda mafunzo Ujerumani je umeleta uthibisho hapa mahakamani unakwenda nje kwa mafunzo
Brenda: Sijaleta
Winniwa: Ni sahini hujawahi pelekea malalamiko yako yoyote kwa kushikiliwa na kunyang’anywa hati yako ya kusafiri
Brenda: Sijasema kitu kama hicho
Winniwa: Hujaileza mahakama ulivyochaguliwa kuwa mkurugenzi wa mawasiliano:
Brenda: Sikuulizwa
Winniwa: Unafahamu nini maani ya neno uasi
Brenda: Kupinga kukataa kwa nguvu kubwa
Winniwa: Kwa hiyo mwenyekiti aliposema uasi alimanisha atatumia nguvu kubwa
Brenda: Aijasema manguvu kubwa nimesema kupinga na kukataa kwa nguvu kubwa sio kwa manguvu makubwa
Winniwa: Unaelewa nini unaposikia kukinukisha
Brenda: Kunukia au kunuka vibaya
Winniwa: Kwa hiyo mlitaka nini kinukie
Brenda: Ukipika pilau kika mtu atajua unapika pilao hivyo tukipinga kwa nguvu kila mtu atajua tunapinga
Winniwa: Waheshimiwa majaji ninaishia hapa nina waaliaka wenzangu waweze kuendelea.
STORI NA DENIS MTIMA | GPL -MAHAKAMANI