
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Septemba 9, 2026, ameshiriki katika Hitma ya kumuombea dua mume wake, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, iliyofanyika Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.
Hitma hiyo imefanyika ikiwa sehemu ya taratibu za kumuombea Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, huku Dkt. Samia akishiriki pamoja na ndugu, jamaa na wananchi katika dua za kumuombea marehemu.
Maalim Hafidh Ameir Hassan alikuwa mume wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
