×

Trump Aahidi Tsh Milioni 12.75 Kwa Kila Raia Mtu Mzima Marekani

Rais wa Marekani, Donald Trump, ameahidi kutoa “dividend” ya dola 5,000 sawa na TSh 12,750,000 kwa kila raia mtu mzima wa Marekani endapo Chama cha Republican kitafanikiwa kudhibiti tena Baraza la Wawakilishi na Seneti katika uchaguzi wa Novemba.

Trump ametoa ahadi hiyo wakati akizungumza katika Mkutano wa Republican uliofanyika Dallas, Texas, akisema malipo hayo yanatokana na kile alichodai kuwa ni mafanikio makubwa ya kiuchumi ya Marekani.

Hata hivyo, Trump amesema sharti pekee la fedha hizo ni kwamba zitumike ndani ya Marekani, huku akisema hazipaswi kutumika katika nchi nyingine.

Trump hakutoa maelezo zaidi kuhusu chanzo cha fedha hizo, namna zitakavyotolewa au muda wa utekelezaji wa mpango huo.

Leave a Comment