Baada ya shabiki kumuomba mfanyabiashara maarufu nchini, Jennifer Bilikwija, anayefahamika zaidi kwa jina la Niffer, atafute namna ya kuwasiliana na mtangazaji na mtayarishaji wa maudhui, Vicent Njau, maarufu kama Kiredio, ili arejee kupost mitandaoni kama alivyokuwa akifanya awali, Niffer ametoa ufafanuzi kuhusu hali yake.

Kupitia Instagram, Niffer alijibu ombi hilo kwa kusema:
“Hayuko sawa kwa sasa but he will be back! Yanini nifiche? Muombeeni ❤️”
Kauli hiyo imeibua mjadala miongoni mwa mashabiki wanaofuatilia kutokuwepo kwa Kiredio kwenye mitandao ya kijamii, huku Niffer akiwaomba kumuombea na kusubiri kurejea kwake.
Hata hivyo, baadhi ya mashabiki wamehusisha kutokuwepo kwa Kiredio mitandaoni na tetesi za kuachana na aliyekuwa mpenzi wake, Vee Dollarz.
Mpaka sasa, taarifa hizo za kuhusisha kutokuwepo kwake mitandaoni na suala hilo zimeendelea kuwa tetesi, huku Niffer akieleza tu kwamba Kiredio “hayuko sawa kwa sasa” bila kufafanua zaidi kuhusu kinachoendelea.

