×

Cardi B Avunja Ukimya Kuhusu Uvumi wa Kurudiana na Offset

RAPA kutoka Marekani, Cardi B, amevunja ukimya kuhusu uvumi unaodai kuwa anajaribu kurejesha uhusiano wake wa kimapenzi na aliyekuwa mume wake, Offset.

Uvumi huo uliibuka Septemba 16, 2026, baada ya mwanamitindo Melanie Jayda, ambaye amewahi kuhusishwa kimapenzi na Offset, kudaiwa kuchapisha ujumbe kwenye mtandao wa X uliosababisha mjadala kuhusu uhusiano wa wawili hao.

Cardi B alijibu madai hayo kupitia chapisho ambalo baadaye lilifutwa, akisisitiza kwamba hakuna ushahidi wa yeye kujaribu kumfuatilia au kurejesha uhusiano na Offset.

“Kamwe maishani mwako, kamwe katika maisha haya… mnaweza kupitia jumbe za simu za jamaa huyo (Offset) au chochote kile… lakini kamwe hutaona nikifanya hivyo. Weka hata mpelelezi binafsi anifuatilie, naapa kwa jina la Yesu, hutapata ushahidi wowote!” aliandika Cardi B.

Kauli hiyo imekuja wakati ambapo historia ya uhusiano wa Cardi B na Offset imekuwa ikifuatiliwa kwa karibu na mashabiki wao.

Julai 2024, Cardi B aliwasilisha ombi la talaka dhidi ya Offset kwa mara ya pili baada ya kuwa pamoja kwa miaka kadhaa.

Wawili hao wana watoto watatu, Kulture, Blossom na Wave, huku mchakato wa talaka yao ukiendelea kukumbwa na changamoto za kisheria.

Leave a Comment