×

Tuchel Awaonya Alexander-Arnold na Palmer Baada ya Kuwaita Tena England

KOCHA wa timu ya taifa ya England, Thomas Tuchel, amewajumuisha tena Trent Alexander-Arnold na Cole Palmer katika kikosi cha

Alexander-Arnold, anayekipiga Real Madrid, amerejea kwenye kikosi cha England kwa mara ya kwanza tangu Juni 2025. Beki huyo alikosa nafasi katika kikosi kilichoshiriki Kombe la Dunia, lakini kiwango kizuri alichoanza nacho msimu huu katika klabu yake kimemsaidia kurejea kwenye timu ya taifa.

Kwa upande wa Palmer, mchezaji huyo wa Chelsea pia ameitwa tena baada ya kukosa Kombe la Dunia kutokana na changamoto za kiwango na utimamu wa mwili msimu uliopita.

Palmer ameanza msimu mpya kwa kiwango kizuri, akiwa amefunga mabao manne na kutoa pasi mbili za mabao katika michezo sita.

Akizungumza kuhusu kurejea kwa wachezaji hao, Tuchel amesisitiza kuwa hakuna anayehakikishiwa nafasi ya kudumu kwenye kikosi, akiwataka kutumia fursa hiyo kuthibitisha uwezo wao.

Kwa Alexander-Arnold, kocha huyo amesema ushindani katika nafasi ya beki wa kulia bado ni mkubwa na mchezaji huyo atalazimika kupigania nafasi yake.

“Anapaswa kupigania nafasi yake,” Tuchel amesema, akisisitiza umuhimu wa kila mchezaji kuonyesha kiwango kinachohitajika ili kuendelea kuwa sehemu ya mipango yake.

England inajiandaa kuanza kampeni yake ya UEFA Nations League kwa mchezo dhidi ya mabingwa wa dunia Spain utakaochezwa katika Uwanja wa Wembley Septemba 26.

Baada ya mchezo huo, England itakutana na Czech Republic na Croatia katika michezo inayofuata, huku Tuchel akitarajiwa kutumia mechi hizo kutathmini kikosi chake na kuandaa timu yenye ushindani.

Stori na Erick Elibariki | GPL -TUDACO

Leave a Comment