×

Wakongwe walivyopagawisha mkesha wa Pasaka, Dar

IMG_5641Staa mkongwe kunako Bongo Fleva, Prince Dully Sykes akikamua jukwaani.

IMG_5663

Sir Juma Nature naye alikuwepo jukwaani kukinukisha.
IMG_5679

Staa mkongwe kutoka Wateule, Jaffarai naye alikuwepo kuzikonga nyoyo za mashabiki.

IMG_5688Afande Sele ‘Baba Tunda’ akiwapigia saluti mashabiki mara baada ya kukamua Wimbo wa Mtazamo.
IMG_5699

Inspector Haroun ‘Babu’ akikamua Wimbo wa Mtoto wa Geti Kali.

IMG_5732

Mmoja wa wasanii wakongwe akikamua jukwaani.

IMG_5771

Kundi linalotikisa tangu kitambo la Mabaga Fresh likikamua jukwaani.

IMG_5804Mkali Soggy Dog Hunter naye alikuwepo kumpa tafu Promota Bonga.
IMG_5868

Mkali wa nyimbo za Uswahilini, Suma G akikamua jukwaani.

IMG_5892

Staa kutoka kundi maarufu la Daz Nundaz, Ferooz akikamua kwa hisia jukwaani.

IMG_5664

Ilikuwa burudani! Staa mkongwe, Sister P akifuatilia jambo kwa makini.

IMG_5705

Kama karambwanda! Nature haokuona aibu baada ya kukata keki ya Promota Bonga kiisha kujisevia.

IMG_5697Nature akiwa katika picha ya pamoja na Mabaga Fresh pamoja na Sister P.
IMG_5635

Mashabiki waliotimba katika shoo hiyo wakishangweka.

IMG_5645

Keki iliyoandaliwa kwaajili ya promota Bonga kutimiza miaka 25 kwenye kazi hiyo.

IMG_5643

….Akijianda kukata keki.

IMG_5718

Akimlisha keki mwanamuziki Juma Nature.

IMG_5719

Akimlisha keki Rich One.

AMA kweli! Ng’ombe hazeeki maini, hivyo ndivyo walivyodhihirisha wasanii wakongwe wa Muziki wa Bongo Fleva mara baada ya kuporomosha bonge la shoo katika Mkesha wa Sikukuu ya Pasaka.

Mkesha huo ulifanyika jana usiku,  katika Ufukwe wa Sunrise uliopo Kigamboni jijini Dar uliendana na sherehe ya kutimiza miaka 25 ya promota maarufu nchini,  Majid Mdoe ‘Promota Bonga’ . Huku wasaniii kama Afande Sele, Dully Sykes, Jaffarai, Suma G, Manzese Crew, Mabaga Fresh,  Zig Zag Crew, Fanani wa Hard Blastaz Crew, Soggy Dog, Inspectour Haruni ‘Babu’ Juma Nature, Sister P, Sold Ground Family Feruzi, Rich One na wengine kibao wakiwakumbusha mashabiki wao kwa muziki uliowahi kufanya vizuri kipindi cha nyuma.

Shoo hiyo iliandaliwa na  na mmoja wa mapromota wakongwe wa muziki huo, Promota Bonga akishirikiana na Kituo cha Redio cha Times FM kilichopo Kawe jijini Dar.

(Na Gabriel Ng’osha/GPL)

Leave a Comment