Aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Bw. Wilson Kabwe.
ALIYEKUWA mbunge wa Nyamagana jijini Mwanza, Ezekiel Wenje aliwahi kumtuhumu aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji hilo, Wilson Kabwe aliyesimamishwa kazi jana na Rais John Pombe Magufuli.
Wenje alitoa tuhuma hizo bungeni kwenye Bunge la 10, Mkutano wa 18, Kikao cha 7 alipoanika namna ambavyo Wilson Kabwe alishiriki katika usifadi wa Mradi wa Ujenzi wa Kliniki jijini humo huku akitoa maelezo kuwa, ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuhusu Special Audit ya mwaka wa fedha 2010/2011 ilipendekeza Kabwe achukuliwe hatua jambo ambalo serikali halikuifanya na badala yake akahamishiwa Dar es Salaam.
Kabla ya kuhamishiwa jijini Dar es Salaam, Kabwe alikuwa ni Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza ambaye alihamishiwa Mwanza akitokea Mbeya baada ya kutuhumiwa kwa ufisadi wa mabilioni kadhaa jijini humo.
LINK==>Rais Magufuli Amtumbua Mkurugenzi Jiji la Dar
JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU:
KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA
INSTAGRAM: @Globalpublishers
TWITTER: @GlobalHabari
FACEBOOK: @GlobalPublishers
SUBSCRIBE YOU TUBE: GlobalPublishers
GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com
HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE: @shigongotz
