Rais John Pombe Magufuli
Makonda amesema kwamba, Kabwe alisaini mikataba miwili, wa 2004 na wa mwaka 2009 ambapo ule wa mwaka 2004 ulipelekwa jiji na ule wa 2009 ukapelekwa kwa mzabuni, hivyo jiji wanajua kuwa basi linatozwa sh. 4000 kwa siku wakati mzabuni anatozwa 8000 kwa siku
Kutokana na maelezo hayo, Mheshimiwa Rais ametangaza kumsimamisha kazi bwana Kabwe ambaye ni Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam na ameagiza vyombo vya dola vianze uchunguzi mara moja ili hatua zaidi za kisheria ziweze kuchukuliwa