Kamanda wa Mkoa wa Tabora, Khamis Issah Sulemani.
WATU wawili waliokuwa wamejeruhiwa kwa risasi wakati wa mapambano na majambazi katika kijiji cha Isila, wilaya ya Uyui mkoa Tabora, wamefariki dunia wakati wakipatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora.
Tukio hilo ambalo lilitokea usiku wa kuamkia juzi Jumapili ambapo majambazi watatu wakiwa na bunduki aina ya SMG, walivamia nyumbani kwa mfanyabiashara wa ng’ombe na kuwajeruhiwa kwa risasi watu wawili huku jambazi mmoja akiuawa wakati wa majibizano ya risasi na polisi na wengine wawili kutokomea kusikojulikana.
Akithibitisha kutokea kwa vifo hivyo vya Bw. Mirija Bapa na ndugu yake Umoja Ubapa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Khamis Selemani amesema kuwa watu hao walizidiwa ghafla wakati wakipata matibabu na kupeleka vifo vyao.
Kamanda Selemani amesema kuwa Jeshi la Polisi bado linaendelea kuwasaka watuhumiwa wawili waliojeruhiwa na polisi katika tukio na kukimbia ambapo ametoa wito kujisalimisha wenyewe ili sheria ifuate mkondo wake.
Hatari; Bi Harusi Aliyetekwa Siku ya Send Off Yake
Basata; Nay wa Mitego Huru Kuendelea na Muziki
Wema na Mama Yake Hii ni Zaidi ya Movi……
Masanja Mkandamizaji Avunja Mbavu Watu Kwenye Harusi Yake
Harusi ya Masanja Ilivyotikisa Jijij la Dar es Salaam………
Harusi ya Masanja Mkandamiza Ilivyoacha Stori Midomoni mwa Watu….
