Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Hamisi Kigwangalla akiwahutubia wananchi waliojitokeza kwenye zoezi hilo la kukusanya michango kwa ajili ya wagonjwa wa kansa wa Hospitali ya Ocean Road.
Baadhi ya watu waliojitokeza jana kwenye zoezi hilo.
NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Hamisi Kigwangalla jana aliongoza matembezi ya kukusanya michango kwa ajili ya kusaidia wagonjwa wanaosumbuliwa na tatizo la kansa katika hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam.
Waziri huyo alisema ili kuondokana na tatizo la kansa ni lazima tuwe na utaratibu wa kupima afya zetu mapema kwani itasaidia kwa wale wenye dalili za mapema za ugonjwa huo kupona kabisa.
“Saratani ya matiti na shingo ya kizazi ikigundulika mapema ikiwa katika hatua za awali mgonjwa anaweza kupona kabisa,” alisema Kingwangala.
Pia alifafanua kuwa ni asilimia kumi tu ya wagonjwa wenye tatizo la kansa wanaofika hospitali mapema, badala yake wengi wao hufika hospitali hatua za mwisho wanapokuwa wamezidiwa.
Aidha aliongeza kuwa serikali imeanza mkakati wa kuzuia na kudhibiti saratani ambao umekwisha zinduliwa na kutoa chanjo kwa wasichana.
Kupata video ya tukio hili tembelea Youtube Chaneli yetu ya Global TV Online, au katika website ya www.globaltvtz.com
Na Hilaly Daud/GPL



