The House of Favourite Newspapers

AMBER LULU KUMZALIA PREZZO!

VIDEO queen ambaye pia anafanya poa kunako Bongo Flevani, Lulu euggen ‘Amber Lulu’ amesema kwa sasa anaona kuwa hakuna cha kusubiri tena zaidi ya kumshauri mpenzi wake, Jackson Makini ‘Prezzo’ wazae mtoto.

Akizungumza na Amani, mrembo huyo alisema, anahitaji kuwa mama sasa kwani mambo ya usichana ameshayafanya sana.

“Nadhani huu ni muda wangu muafaka wa kuzaa, namshauri anayenimiliki tupate hata mapacha wa harakaharaka maana usichana nimeshafanya sana, nataka kuwa mama sasa  nibebe mtoto wangu ninyonyeshe,” alisema Amber Lulu

Comments are closed.