Matokeo ya Mtihani Kidato cha Sita, Ualimu 2021
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Dkt Charles Msonde anatangaza matokeo ya Mitihani ya Kidato cha Sita na Ualimu iliyofanyika Mei 2021. Matokeo hayo yanatangaziwa Zanzibar.
Dkt. Charles Msonde amesema ufaulu katika matokeo ya mtihani wa kidato cha sita kwa mwaka 2021 umepanda kwa asilimia 0.11 huku shule za Serikali zikichuana vikali na za binafsi.