The House of Favourite Newspapers

Mambo Magumu Kwa Uchebe

0

Kocha Mkuu wa Abaluhya Football Club Leopards Sports Club ‘AFC Leopards’ ya Kenya, Patrick Aussems raia wa Ubelgiji ana wakati mgumu katika ligi ya Kenya.

Aussems ambaye amewahi kuhudumu katika Klabu ya Simba, kwenye msimamo wa ligi, Leopards iko nafasi ya 16 kati ya timu 18 huku ikipoteza mechi 5 kati ya mechi saba ilichochea hadi sasa, ameshinda mechi moja na kutoa sare moja.

Matokeo ya jumla hadi sasa ni kama ifuatavyo.

AFC Leopards 1-0 Tusker
KCB 0-0 AFC Leopards
AFC Leopards 0-1 Gor Mahia
Bandari 2-1 AFC Leopards
AFC Leopards 0-2 Ulinzi Stars
Sofapaka 1-0 AFC Leopards
Bidco United 1-0 AFC Leopards.
Matokeo haya unaweza kuyaweka kwenye rekodi ya WDLLLLL.

Aussems maarufu kama Uchebe alichukuliwa na klabu hiyo kwa matumaini ya kuirudisha kwenye hadhi yake ikiwa pamoja na kutwaa ubingwa wa Kigi Kuu ya Kenya ambao mara ya mwisho walishinda mwaka 1998 wakiwa chini ya kocha mtanzania, Sunday Kayuni.

Leave A Reply